logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Seneta Linturi aachiliwa kwa bondi ya Sh5M katika kesi ya uchochezi

Hakimu Mkuu wa Nakuru Edna Nyaloti ameamuru seneta huyo kutowasiliana na mashahidi kwa njia yoyote ile iwe ni moja kwa moja au kupitia wakala.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 January 2022 - 08:08

Muhtasari


•Hakimu Mkuu wa Nakuru Edna Nyaloti ameamuru seneta huyo kutowasiliana na mashahidi kwa njia yoyote ile iwe ni moja kwa moja au kupitia wakala.

Seneta wa Meru Mithika Linturi ameachiliwa kwa bondi ya Sh5 milioni na mdhamini wa kiasi sawa na hicho na dhamana mbadala ya Sh2milioni pesa taslimu.

Seneta wa Meru Mithika Linturi ameachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu shilingi milioni mbili au mdhamini wa kiasi cha shilingi milioni 5 kutokana na matamshi yake ya chuki aliyotoa mjini Eldoret.

Hakimu Mkuu wa Nakuru Edna Nyaloti ameamuru seneta huyo kutowasiliana na mashahidi kwa njia yoyote ile iwe ni moja kwa moja au kupitia wakala.

Nyaloti alisema hakuna ushahidi wa kutosha kuzuia uhuru wa mshtakiwa kabla ya kufunguliwa mashtaka.

Amesema serikali ina mitambo ya kuendelea na uchunguzi bila kumnyima mwandani huyo wa naibu rais uhuru wake.

Hali kadhalika amesema serikali inaweza kumfuatilia seneta Linturi na hata kuingilia mawasiliano yake.

Linturi alikamatwa siku ya Jumapili kufuatia matamshi ambayo alitoa alipokuwa anahutubia wafuasi wa naibu rais William Ruto mjini Eldoret.

Matamshi ya Linturi 'madoadoa' yalikosolewa na yanaendelea kukosolewa sana na Wakenya ikiwemo viongozi wa hadhi mbalimbali.

"Sisi tunataka kuwa kwa serikali inayokuja lakini nawaambia watu wa Uasin Gishu msicheze na Kenya na kile nawaomba ni kwamba madoadoa yale mliyonayo hapa muweze kuondoa. Hatuwezi kuwa tukisimama na William Ruto kule Mt Kenya na mko na wengine hapa hawasikii na hawawezi ungana naye...". Linturi alisikika akisema.

Mnamo Jumatatu naibu rais William Ruto aliomba radhi kufuatia matamshi hayo ya mwandani wake.

Kesi ya Linturi itatajwa tena mnamo Januari 26.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved