logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Miguna Miguna amkosoa Ruto kwa kuomba msamaha kufuatia matamshi ya Linturi 'madoadoa'

Kulingana na Miguna, mateso ya seneta Linturi ni ya kisiasa na haikuwa na haja naibu rais William Ruto kuomba msamaha.

image
na Radio Jambo

Habari11 January 2022 - 05:43

Muhtasari


•Kulingana na Miguna, mateso ya seneta Linturi ni ya kisiasa na haikuwa na haja naibu rais William Ruto kuomba msamaha.

Wakili na mwanasiasa maarufu Miguna Miguna ametoa maoni yake kuhusiana na matamshi ya seneta wa Meru Mithika Linturi 'madoadoa' .

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Miguna amesema matamshi ya mwandani huyo wa naibu rais yalikuwa maoni yasiyohitaji udhibiti wa serikali na hayakumaanisha uhalifu.

Kulingana na Miguna, mateso ya seneta Linturi ni ya kisiasa na haikuwa na haja naibu rais William Ruto kuomba msamaha.

"Maoni ya Mithika Linturi ya "madoadoa" hayakuwa ya kihalifu na ni hotuba iliyolindwa. Mateso yake ni ya kisiasa. Hakuna sababu kabisa kwa nini @WilliamsRuto ameomba msamaha isipokuwa kwamba anathamini mamlaka juu ya kanuni" Miguna aliandika.

Wakili huyo ameagiza hatua sawa kuchukuliwa dhidi ya wachochezi wote bila ubaguzi wa aina yoyote kwa misingi ya kisiasa.

Miguna pia alihimiza Ruto na kinara wa ODM Raila Odinga kupigania haki ya uchaguzi na kuhakikisha uchaguzi wa mwezi Agosti utakuwa huru, wa haki na wa kuaminika.

"DP William Ruto, Raila Odinga na wafuasi wao wanapaswa kupigania haki ya uchaguzi na kuhakikisha kwamba uchaguzi wa 2022 ni huru, wa haki, unaoweza kuamini na ambao unaweza kuthibitishwa" Alisema Miguna.

Mnamo Jumatatu naibu rais William Ruto alipokuwa anahutubia wafuasi aliomba msamaha kufuatia matamshi yaliyotolewa na Linturi mjini Eldoret Jumamosi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved