logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila azindua miradi ya maji Taita -Taveta

Waziri mkuu huyo wa zamani atafanya mkutano wa barazani ambapo atauza sera zake na kunadi muungano wa Azimio la umoja.

image
na Radio Jambo

Burudani14 January 2022 - 10:10

Muhtasari


• Kiongozi huyo wa muungano wa Azimio la Umoja atazindua rasmi miradi mbali mbali ya maji iliyofadhiliwa na serikali ya kaunti ya Taita Taveta. 

• Raila atahutubia mikutano ya hadhara katika maeneo ya Overseer na Mwatate.

 

kinara wa ODM Raila Odinga

  Kinara wa Odm Raila Odinga ameanza ziara yake katika kaunti ya Taita Taveta. Raila anafanya ziara ya siku moja katika kaunti hiyo. 

Kiongozi huyo wa muungano wa Azimio la Umoja akiwa katika ziara hiyo atazindua rasmi miradi mbali mbali ya maji iliyofadhiliwa na serikali ya kaunti ya Taita Taveta. 

Waziri mkuu huyo wa zamani atafanya mkutano wa barazani ambapo atauza sera zake na kunadi muungano wa Azimio la umoja.

Katika mkutano huu atakutana na makundi mbali mbali kutoka kaunti ya Taita Taveta.  Miradi ya maji inayozinduliwa inapatikana katika maeneo ya Maktau na Overseer.

Maeneo haya yamekuwa yakikabiliwa na changomoto za maji tangu jadi na miradi hii ni afueni kubwa kwa wenyeji. 

Raila atahutubia mikutano ya hadhara katika maeneo ya Overseer na Mwatate. Katika hotuba yake anatarajiwa kuhubiri ujumbe wa amani, upendo, matumaini na ufanisi chini ya kampeini zake za Azimio la Umoja. 

Katika ziara hiyo Raila anaandamana na wenyeji wake Gavana Granton Samboja, Mbunge wa Mwatate Andrew Mwadime, Naibu kinara wa wengi bungeni Naomi Shaban, Seneta wa Taita-Taveta Jones Mwaruma miongoni mwa viongozi wengine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved