logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 5 wamefariki, watatu wajeruhiwa katika ajali ya barabara kuu ya Namanga-Kajiado

Polisi walisema wengine watatu waliachwa katika hali mbaya baada ya ajali hiyo katika eneo la Ilbisi.

image
na

Habari22 January 2022 - 10:10

Muhtasari


  • Watu 5 wamefariki, watatu kujeruhiwa katika ajali ya barabara kuu ya Namanga-Kajiado
  • Miili ya marehemu imehamishiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kajiado, huku waliojeruhiwa wakilazwa katika kituo kimoja
Ajali

Watu watano walipoteza maisha yao Jumamosi asubuhi baada ya magari mawili kugongana kwenye barabara kuu ya Namanga-Kajiado.

Polisi walisema wengine watatu waliachwa katika hali mbaya baada ya ajali hiyo katika eneo la Ilbisi.

Magari hayo yalikuwa yakielekea pande tofauti wakati wa ajali hiyo.

Probox, iliyokuwa ikielekea Ilbisil ilikuwa na watu kadhaa na wanne kati yao walikufa papo hapo huku wengine wakipata majeraha mabaya, polisi waliotembelea eneo la tukio walisema.

Miili ya marehemu imehamishiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kajiado, huku waliojeruhiwa wakilazwa katika kituo kimoja.

Polisi walisema wanachunguza tukio hilo.

Imejiri wakati ambapo maafisa wanasema ajali hizo zinaongezeka ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana tangu mwaka mpya.

Kufikia sasa zaidi ya watu 270 wameuawa katika ajali tangu mwaka mpya, kamanda wa trafiki Mary Omari alisema ikilinganishwa na 201 waliofariki kipindi kama hicho mwaka wa 2021.

Wengi wao ni watembea kwa miguu.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved