logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jaguar ajiunga na Chama cha UDA

Habari za kuhamia  kwenye chama hicho zilitangazwa kwenye ukurasa wa Twitter, Jumatatu asubuhi, na chama cha UDA .

image
na

Yanayojiri24 January 2022 - 07:52

Muhtasari


•Habari za kuhama kwake  zilitangazwa kwenye ukurasa wa Twitter, Jumatatu asubuhi, na chama cha UDA .

•Hatua ya Jaguar inajiri siku chache baada ya mcheshi Jasper Muthomi, almaarufu Mc Jessy, kutangaza kuwa atawania kiti cha Imenti Kusini kwa tikiti ya chama cha UDA

Mheshimiwa Chalres Njagua akiwa na Naibu Rais Ruto

Mbunge wa Starehe Chalres Njagua almaarufu Jaguar amejiunga rasmi na  chama cha Naibu Rais William Ruto, UDA.

Habari za kuhama kwake  zilitangazwa kwenye ukurasa wa Twitter, Jumatatu asubuhi, na chama hicho .

"The Hustler Nation inamkaribisha Mhe. Charles Kanyi Njagua Mbunge wa Starehe. Chama kinazidi kukua kwa kasi na mipaka huku viongozi wengi wakichagua kujiunga na kikosi cha washindi."

Hatua ya Jaguar inajiri siku chache baada ya mcheshi Jasper Muthomi, almaarufu Mc Jessy, kutangaza kuwa atawania kiti cha Imenti Kusini kwa tikiti ya chama cha UDA.

Mcheshi huyo alithibitisha Jumatano kwamba amejiunga rasmi na chama kinachongoozwa na  Ruto baada ya mashuriano mapana na wakazi wa eneo hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved