logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi wa chuo kikuu akamatwa kwa kuuza mitihani ya KCPE na KCSE

Mshukiwa aliwadai watahiniwa shilingi 1,600 - 2,600 kwa mitihani mbalimbali.

image
na Radio Jambo

Habari11 March 2022 - 06:57

Muhtasari


•Brighton alipatikana na na karatasi bandia za mitihani hiyo huku akiwa amehifadhi zingine kwenye simu yake ya mkono.

Wapepelezi wa DCI wamemtia mbaroni mwanafunzi wa ekonomia katika chuo kikuu cha Zetech kwa madai ya kuuza mitihani bandia ya KCPE na KCSE.

Kupitia taarifa iliyotolewa Ijumaa asubuhi, DCI imesema Oscar Brighton ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu alikamatwa Alhamisi na maajenti wa KNEC baada ya kuhusishwa na uhalifu huo.

Brighton alipatikana na na karatasi kadhaa bandia za mitihani hiyo huku akiwa amehifadhi zingine kwenye simu yake ya mkono.

Kulingana na DCI, mshukiwa alikuwa ameunda vikundi vya WhatsApp ambapo alikuwa anaendeleza biashara hiyo laghai.

Mshukiwa aliwadai watahiniwa shilingi 1,600 - 2,600 kwa mitihani tofauti. 

Brighton ambaye si mhalifu wa mara ya kwanza anatarijiwa kufikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa kukiuka sheria za mitihani ya kitaifa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved