logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa atiwa mbaroni kwa kuvamia polisi mwanamke na kuiba sare yake Mombasa

Tukio hilo lilitokea katika eneo la Changamwe takriban wiki moja iliyopita.

image
na Radio Jambo

Habari06 April 2022 - 06:26

Muhtasari


•Mshukiwa alikamatwa katika eneo la Makupa na sare ya polisi iliyoibiwa kutoka kwa afisa huyo wa kike ikapatikana kwake.

crime scene 1

Polisi jijini Mombasa wanamzuilia mshukiwa mmoja wa ujambazi aliyemvamia na kumpora polisi mwanamke sare yake na vitu vingine vya thamani.

Mshukiwa alikamatwa katika eneo la Makupa na sare ya polisi iliyoibiwa kutoka kwa afisa huyo wa kike ikapatikana kwake.

Tukio hilo lilitokea katika eneo la Changamwe takriban wiki moja iliyopita.

Polisi wanasema wanaendelea kuwasaka washukiwa zaidi waliohusika kwenye tukio hilo la wizi ambalo lilitokea wakati afisa huyo alikuwa akielekea kwenye kituo cha basi ili kuenda kazini.

Mshukiwa huyo alitarajiwa mahakamani kujibu mashtaka mbalimbali yakiwamo ya wizi wa kutumia nguvu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved