logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi wasaka jamaa aliyemjeruhi mkewe kwa nyundo na kisu - Kwale

Mwanaume huyo ambaye ni mwalimu alitoroka na anasakwa.

image
na Radio Jambo

Habari05 May 2022 - 07:40

Muhtasari


• Namubuya, 29, anaendelea kupata nafuu katika hospitali ya Kaunti Ndogo ya Lunga Lunga akiwa katika hali shwari. 

 

Crime scene

Maafisa wa upelelezi katika kaunti ya Kwale wanamsaka mwanamume anayedaiwa kumjeruhi mkewe ambaye waliachana naye kwa nyundo na kisu usiku wa kuamkia leo (Alhamisi). 

James Kimeu anasemekana kumdunga kisu Caren Namubuya kifuani na kumpiga kichwani mara kadhaa kwa nyundo kabla ya kukimbia, na kumwacha akiwa amepoteza fahamu kwenye dimbwi la damu. 

Mkurugenzi wa DCI George Kinoti alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa wawili hao walitengana kabla ya Kimeu, 35, kumwalika Namubuya nyumbani kwake kwa nia ya kutafuta maridhiano. 

“Hata hivyo, Kimeu alifunga mlango kwa kufuli na kumgeukia mwanamke huyo kwa kisu cha jikoni na nyundo,” Kinoti alisema. 

Kinoti alisema majirani waliosikia zogo hilo waliingia kwa nguvu ndani ya nyumba hiyo na kumpata mwathiriwa akiwa amelala sakafuni kwenye dimbwi la damu. 

Namubuya, 29, anaendelea kupata nafuu katika hospitali ya Kaunti Ndogo ya Lunga Lunga akiwa katika hali shwari. 

“Mwanaume huyo ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi ya Menzamwenye, hata hivyo alifanikiwa kutoroka na tangu sasa wapelelezi wameanza msako,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved