logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DCI yapata naibu mkurugenzi mpya Hamis Masa

Masa ni mkurugenzi wa muda mrefu wa ANU na uteuzi wake unaonekana kama zawadi kwa kazi yake.

image
na

Habari06 May 2022 - 15:26

Muhtasari


• Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya Hamis Masa alipandishwa cheo kuchukua wadhifa wa naibu DCI katika mabadiliko yaliyotangazwa Alhamisi. 

• Hatua hii inafuatia kustaafu kwa Joseph Ashmalla kutoka kwa huduma baada ya kufikia umri wa kustaafu. 

Naibu mkurugenzi mpya wa Idara ya Upelelezi wa Jinai nchini (DCI) ametajwa katika mabadiliko yaliyotangazwa na mkurugenzi George Kinoti. 

Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya Hamis Masa alipandishwa cheo kuchukua wadhifa wa naibu DCI katika mabadiliko yaliyotangazwa Alhamisi. 

Hatua hii inafuatia kustaafu kwa Joseph Ashmalla kutoka kwa huduma baada ya kufikia umri wa kustaafu. 

Katika mabadiliko hayo, mkuu wa DCI katika Kitengo cha Polisi wa Viwanja vya Ndege (KAPU) Bernard Nyakwaka alihamishwa na sasa mkuu wa DCI katika kanda ya Kati Jinai (RCIO) akibadilishana na Geoffrey Kathurima. 

Mkurugenzi mpya wa wafanyikazi katika makao makuu ya DCI atakuwa Gideon Kibunja. Kibunja alichukua nafasi kutoka kwa Dkt. Wanderi Mwangi ambaye alihamishwa hadi Shirika la Reli na kuteuliwa afisa mkuu wa upelelezi wa Jinai (CCIO). 

Mkurugenzi mpya wa mafunzo atakuwa CCIO wa Railway anayeondoka John Kamau huku Samuel Kobina akihamishwa kutoka chuo cha DCI, na kuteuliwa mkuu wa DCI kaunti ndogo ya Langata. Kinoti alitaja mabadiliko hayo kuwa ya kawaida yanayolenga kuimarisha utendakazi katika idara hiyo. 

Masa ni mkurugenzi wa muda mrefu wa ANU na uteuzi wake unaonekana kama zawadi kwa kazi yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved