logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Muturi atupilia mbali hati za kunyakua ardhi dhidi ya DP Ruto

Muturi alisema suala hilo limefungwa na hakutakuwa na mjadala wowote kulihusu.

image
na

Habari10 May 2022 - 12:43

Muhtasari


• Muturi alimwagiza karani wa Bunge la Kitaifa Michael Sialai kuondoa hati hizo na kumrudishia Gedi haraka iwezekanavyo. 

the star

Muturi atupilia mbali hati za kunyakua ardhi dhidi ya DP Ruto  Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi mnamo siku ya Jumanne alitupilia mbali stakabadhi zilizowasilishwa na Mbunge wa Wajir Fatuma Gedi kuthibitisha madai yake kuwa naibu rais William Ruto ni mnyakuzi wa ardhi. 

Muturi alisema kwamba mbunge huyo hakufuata sheria kanuni zilizowekwa za kuwasilisha stakabadhi, na kumkosoa Gedi kwa kujaribu kumjadili Ruto kupitia mlango wa nyuma. 

Muturi alimwagiza karani wa Bunge la Kitaifa Michael Sialai kuondoa hati hizo na kumrudishia Gedi haraka iwezekanavyo. 

"Kwa kuzingatia uamuzi huu, suala hilo limefungwa na hakutakuwa na mjadala wowote kulihusu," Muturi aliagiza.  

Spika alisema utaratibu wa hoja kama hayo ni kwamba mbunge yeyote mwenye madai hayo aweke mezani nyaraka na spika athibitishe kuruhusiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved