logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru akutana na Ruto katika mkutano wa baraza la mawaziri

Hii ni mara ya kwanza kwa Uhuru kuitisha mkutano wa baraza la mawaziri katika kipindi cha mwaka mmoja.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri12 May 2022 - 11:57

Muhtasari


• Wawili hao walikutana katika Ikulu ya Nairobi, ambapo kiongozi wa taifa aliongoza mkutano huo.

Rais Uhuru Kenyatta akiongoza baraza la Mawaziri Alhamisi 5/12/2022

Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto walikutana siku ya Alhamisi kwa kikao cha Baraza la Mawaziri.

Wawili hao walikutana katika Ikulu ya Nairobi, ambapo kiongozi wa taifa aliongoza mkutano huo.

Taarifa kutoka Ikulu ilisema masuala ya umuhimu wa kitaifa na kimataifa yalikuwa yajadiliwa wakati wa mkutano huo.

"Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta leo yuko Ikulu, Nairobi, akiongoza kikao kamili cha Baraza la Mawaziri ambapo masuala kadhaa ya umuhimu wa kitaifa na kimataifa yatajadiliwa," ilisoma tweet ya ikulu.

Hii pia ni mara ya kwanza kwa Uhuru kuitisha mkutano wa baraza la mawaziri katika kipindi cha mwaka mmoja.

Baraza la Mawaziri linatarajiwa kuandaa kikao kila Alhamisi kujadili masuala muhimu yanayohusu serikali.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved