Raila afanya mashauriano na Museveni ikulu ya Entebbe

Muhtasari

• Raila ambaye anachukuliwa kuwa mmoja wa wagombeaji wa wanaoangaliwa katika uchaguzi wa urais wa Agosti 9, alimtembelea Rais Museveni Alhamisi jioni.

• Odinga anatarajiwa kukabiliwa na changamoto kubwa kutoka kwa Naibu Rais William Ruto anaewania kupitia tiketi ya muungano wa Kenya Kwanza.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni akishauriana na kiongozi wa Azimio Raila Odinga
Rais wa Uganda Yoweri Museveni akishauriana na kiongozi wa Azimio Raila Odinga
Image: RAILA ODINGA/TWITTER

Rais wa Uganda Yoweri Museveni anasema mazungumzo na mgombea urais wa Kenya, Raila Odinga yaliyofanyika Ikulu ya Entebbe yaligusia masuala yanayohusu nchi hizo mbili jirani.

Bw Odinga, ambaye anachukuliwa kuwa mmoja wa wagombeaji wa wanaoangaliwa katika uchaguzi wa urais wa Agosti 9, alimtembelea Rais Museveni jana jioni.

Katika ujumbe wake wa Twitter kuhusu mkutano huo, Bw Odinga alisema wamejadili historia ya pamoja ya nchi zao inayolenga kuimarisha uhusiano wa siku zijazo.

Siku mbili zilizopita, Odinga alikuwa Sudan Kusini ambako alikutana na Rais Salva Kiir na kuzindua Daraja la Uhuru la kilomita 3.6 linalotarajiwa kurahisisha usafirishaji wa bidhaa katika Mto Nile.

Orodha ya wagombea urais 55 wameidhinishwa kugombea katika uchaguzi wa Kenya.

Odinga anatarajiwa kukabiliwa na changamoto kubwa kutoka kwa Naibu Rais William Ruto anaewania kupitia tiketi ya muungano wa Kenya Kwanza.

Uchaguzi wa Kenya ni muhimu katika kanda hiyo kwa sababu ndio mahali pa kuingizia bidhaa kutoka nchi zisizo na bandari kama vile Uganda, Sudan Kusini na Kongo DR.

Eneo hilo litakuwa na wasiwasi kutokana na uchaguzi uliokumbwa na ghasia wa mwaka 2007 ambao uliathiri uchumi wao.