logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kwa nini nimezuiwa kushiriki uchaguzi? - Kigame auliza IEBC

Mwanamuziki huyo ametilia shaka uadilifu wa IEBC akitaja kwamba alitii mahitaji yote

image
na Radio Jambo

Habari06 June 2022 - 09:33

Muhtasari


  • Mwanamuziki huyo ametilia shaka uadilifu wa IEBC akitaja kwamba alitii mahitaji yote ambayo tume hiyo iliweka
Mgombea urais Reuben Kigame akihutubia wanahabari nje ya jumba la Anniversary Tower Nairobi, baada ya jaribio lake kukutana na mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati kugonga mwamba./WILFRED NYANGARESI

Mgombea Huru wa Urais Reuben Kigame amepinga Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kueleza ni kwa nini alizuiwa kushiriki katika Uchaguzi Mkuu ujao wa Agosti 9.

Akitumia ukurasa waketwitter mnamo Jumatatu, Juni 6, Kigame alieleza kwa kina matukio yaliyojiri kati ya Mei 16 alipotangazwa kwenye gazeti la serikali kama mgombea Urais hadi Mei 30 alipofungiwa nje ya kinyang'anyiro hicho.

Mwanamuziki huyo ametilia shaka uadilifu wa IEBC akitaja kwamba alitii mahitaji yote ambayo tume hiyo iliweka lakini bado akakataliwa kwa sababu zisizojulikana.

"Wakati wanaotaka kugombea wameondolewa kwa kutokuwa na saini na nakala za vitambulisho, ninazo lakini bado naonekana kutofuata sheria, marafiki kwanini nazuiwa kugombea katika uchaguzi wa Agosti? Kwa nini nchi hii inanichukulia hivi? Mtu aniambie kwa nini,"Aliuliza KIgame.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved