logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa gavana wa Bomet Isaac Rutto ampoteza mama yake

Koech pia alitangaza kuwa chama kimesimamisha kampeni ili kuomboleza na familia

image
na Radio Jambo

Habari14 June 2022 - 13:07

Muhtasari


  • Aliyekuwa gavana wa Bomet Isaac Rutto ampoteza mama yake

Mamake aliyekuwa Gavana wa Bomet Isaac Rutto ameaga dunia.

Katika taarifa Jumanne, katibu mkuu wa Chama Cha Mashinani Albert Koech alisema Mama Jane Tirop alifariki alipokuwa akitibiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Moi mjini Eldoret.

"Ni kwa moyo mzito kutangaza kifo cha  Mama Jane Tirop, mama mpendwa kwa Gavana Isaac Ruto, Kiongozi wa Chama cha CCM. Mama Jane alienda kuwa na Bwana Jumanne asubuhi, 14 Juni 2022 katika MTRH Eldoret, " alisema.

"Kwa niaba ya Chama Cha Mashinani, napenda kufikisha salamu za rambirambi kwa familia ya Chama chetu katika kipindi hiki kigumu."

Koech pia alitangaza kuwa chama kimesimamisha kampeni ili kuomboleza na familia ya kiongozi wao wa chama.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved