logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kenyatta wakamatwa kwa kudukua akaunti za watu na kuiba pesa

Washukiwa wanadaiwa kuzitumia hela walizoiba kuishi kifahari, kutumbuiza wanadada na kununua mali.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri16 June 2022 - 04:58

Muhtasari


•Wawili hao walikuwa pamoja na wanawake wawili walipokamatwa katika nyumba yao ya kifahari.

•Inaripotiwa kuwa washukiwa wamekuwa wakiziandamana zaidi akaunti za watu wanaishi nje ya nchi.

Wapelelezi wa DCI wanawazuilia wanafunzi wawili wa Chuo Kikuu cha Kenyatta kwa madai ya wizi wa pesa kupitia udukuzi wa kadi za benki.

Francis Maina ,26, na Zellic Alusa ,25, walikamatwa Jumatano katika eneo la Mimilani, mjini Nakuru baada ya kuwa kwenye rada za polisi kwa siku kadhaa. Wawili hao walikuwa pamoja na wanawake wawili walipokamatwa katika nyumba yao ya kifahari.

Inaripotiwa kuwa wamekuwa wakidukua kadi za benki za watu kisha kuzitumia kununua bitcoins. Baada ya kununua bitcoins, washukiwa wanadaiwa kuzibadilisha tena kuwa pesa za Kenya kwa ajili ya matumizi.

Kitengo cha DCI kimeripoti kuwa washukiwa wamekuwa wakidukua akaunti za watu kutumia akaunti bandia za barua pepe walizotengeneza.

Inaripotiwa kuwa washukiwa wamekuwa wakiziandamana zaidi akaunti za watu wanaishi nje ya nchi.

Baada ya kufanikiwa washukiwa wanadaiwa kuzitumia hela walizoiba kuishi kifahari, kutumbuiza wanadada na kununua mali.

Pale nyumbani kwa washukiwa polisi waliweza kupata hati za mauzo ya jumba la Ksh850,000 lililo katika eneo la Juja, Kiambu.

Pia walifanikiwa kupata kompyuta tano za mkononi, simu nne, vifaa viwili vya Wi-Fi, kadi kadhaa za simu kati ya vitu vingine.

Usalama wa kidijitali umeboreshwa nchini Kenya baada ya rais Kenyatta kuagiza kuimarishwa kwa maabara ya uchunguzi wa kidijitali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved