logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Miguna awashtaki Matiang'i na Kibicho kufuatia kufurushwa kwake, adai fidia ya Bilioni 1.7

Kesi hiyo iliwasilishwa katika Mahakama ya Ontario, nchini Kanada.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 June 2022 - 02:56

Muhtasari


•Miguna alisema baada ya kukamatwa, alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka kinyume na Katiba ya Kenya na kuteswa kwa muda wa siku sita.

•Alisema fidia hiyo itagharamia madhara yaliyotokana na kufurushwa kwake.

Miguna Miguna afurushwa kutoka Kenya mnamo Machi 2018

Wakili Miguna Miguna amewasilisha kesi dhidi ya Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i akitaka alipwe fidia ya Sh1.7 bilioni.

Kesi hiyo iliwasilishwa katika Mahakama ya Ontario, nchini Kanada siku ya Alhamisi.

Alisema fidia hiyo itagharamia madhara yaliyotokana na kufurushwa kwake, ambayo ni pamoja na kushambuliwa, kuharibiwa jina na kuwekwa kizuizini kinyume cha sheria miongoni mwa mengine.

Wengine walioshitakiwa katika kesi hiyo ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Karanja Kibicho na makampuni ya kimataifa; Sitel Operating Corporation and Refinitiv Limited. 

Miguna alisema kufurushwa kwake mwezi Februari 2018 kuliharibu sifa yake.

“Mlalamikaji anadai kwa pamoja na kwa kiasi kikubwa fidia ya kuwekwa kizuizini kinyume cha sheria, mateso, shambulio na kudhulumiwa kwa jumla ya Sh1.1 bilioni na fidia nyingnine ya jumla ya Sh587,050,000 kwa kuharibiwa jna, " hati ya mahakama iliyoonyeshwa na Miguna ilisoma.

Miguna aliiambia Mahakama kuwa alikuwa wakili bora wa Ontario kwa zaidi ya miaka 27, vile vile mwandishi, mtoa maoni, wakili na mwanaharakati wa haki za binadamu nchini Kenya, na mkazi wa Mkoa wa Ontario.

Wakili huyo anadai zaidi fidia ya Sh234,820,000 kwa ukiukaji wa faragha alioufanya wakati wa kukamatwa kwake nyumbani kwake kabla ya kufukuzwa nchini.

Miguna alisema baada ya kukamatwa, alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka kinyume na Katiba ya Kenya na kuteswa kwa muda wa siku sita.

"Siku ya sita, maajenti wa usalama wa Kenya waliokuwa na silaha nzito chini ya amri ya moja kwa moja ya washtakiwa Matiang'i na Kibicho walimfukuza mlalamikaji kwa nguvu hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (ambao unajulikana kama "JKIA") jijini Nairobi na kumlazimisha kuingia. ndege ya KLM kuelekea Amsterdam," kesi hiyo ilisomeka zaidi.

Pia alisema mara kwa mara, Matiang'i na Kibicho walihutubia wanahabari wakichukua jukumu la kuzuiliwa kwake na kushtakiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved