Mwanahabari mkongwe Joe Kadhi amefariki dunia

Familia yake ilisema mwanahabari huyo mkongwe atazikwa Alhamisi (Leo) kwa mujibu wa imani ya Kiislamu.

Muhtasari

• Kadhi alikuwa na taaluma ya hadhi ya juu na kufanya kazi katika kampuni ya Nation Media Group kama mhariri mkuu.

Mwanahabari mkongwe Joe Kadhi
Mwanahabari mkongwe Joe Kadhi

Kadhi alifariki siku ya Jumatano, alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi.

Familia yake ilisema mwanahabari huyo mkongwe atazikwa Alhamisi (Leo) kwa mujibu wa imani ya Kiislamu.

Kadhi alikuwa na taaluma ya hadhi ya juu na kufanya kazi katika kampuni ya Nation Media Group kama mhariri mkuu.

Joe kadhi na naibu Afisa Mkuu Mtendaji wa Baraza la Vyombo vya Habari nchini (MCK) Victor Bwire katika hafla ya awali.
Joe kadhi na naibu Afisa Mkuu Mtendaji wa Baraza la Vyombo vya Habari nchini (MCK) Victor Bwire katika hafla ya awali.
Image: HISANI

Pia alikuwa msomi na alifundisha uandishi wa habari katika Chuo Kikuu cha Nairobi, Chuo Kikuu cha Addis Ababa na Chuo Kikuu cha USIU.

Joe kadhi
Joe kadhi
Image: HISANI

Kadhi, ambaye alipokea tuzo ya mafanikio ya maisha katika Tuzo za Kila Mwaka za Uandishi wa Habari za Baraza la Habari nchini (MCK) mwaka 2015, awali alikuwa mwenyekiti wa bodi ya wahariri ya jarida la Media Observer.