logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanahabari mkongwe Joe Kadhi amefariki dunia

Alifundisha uanabari katika Chuo Kikuu cha Nairobi, Addis Ababa na Chuo na USIU.

image
na Radio Jambo

Burudani30 June 2022 - 04:49

Muhtasari


• Kadhi alikuwa na taaluma ya hadhi ya juu na kufanya kazi katika kampuni ya Nation Media Group kama mhariri mkuu.

Mwanahabari mkongwe Joe Kadhi

Kadhi alifariki siku ya Jumatano, alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi.

Familia yake ilisema mwanahabari huyo mkongwe atazikwa Alhamisi (Leo) kwa mujibu wa imani ya Kiislamu.

Kadhi alikuwa na taaluma ya hadhi ya juu na kufanya kazi katika kampuni ya Nation Media Group kama mhariri mkuu.

Joe kadhi na naibu Afisa Mkuu Mtendaji wa Baraza la Vyombo vya Habari nchini (MCK) Victor Bwire katika hafla ya awali.

Pia alikuwa msomi na alifundisha uandishi wa habari katika Chuo Kikuu cha Nairobi, Chuo Kikuu cha Addis Ababa na Chuo Kikuu cha USIU.

Joe kadhi

Kadhi, ambaye alipokea tuzo ya mafanikio ya maisha katika Tuzo za Kila Mwaka za Uandishi wa Habari za Baraza la Habari nchini (MCK) mwaka 2015, awali alikuwa mwenyekiti wa bodi ya wahariri ya jarida la Media Observer.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved