logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Uhuru amuomboleza aliyekuwa waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe

Waziri Mkuu wa zamani Abe, ambaye alistaafu mwaka wa 2020, alitembelea Nairobi mwaka wa 2016

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 July 2022 - 12:05

Muhtasari


  • Rais alionyesha kushtushwa na kifo cha ghafla cha kiongozi huyo wa zamani wa Japan na kumtaja kama rafiki na mshirika wa maendeleo wa taifa la Kenya

Rais Uhuru Kenyatta ameungana na viongozi wa dunia kuomboleza aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe aliyefariki siku ya Ijumaa baada ya kupigwa risasi kwenye mkutano wa kampeni za kisiasa.

Rais alionyesha kushtushwa na kifo cha ghafla cha kiongozi huyo wa zamani wa Japan na kumtaja kama rafiki na mshirika wa maendeleo wa taifa la Kenya.

Katika ujumbe wake wa rambi rambi ulisoma;

"Inashangaza sana na kwa kiasi fulani haiaminiki kujua kuhusu kifo cha rafiki yangu, na mmoja wa washirika wakuu wa maendeleo wa Kenya, Waziri Mkuu wa zamani Shinzo Abe, katika tukio la kupigwa risasi kikatili," Uhuru alisema.

Waziri Mkuu wa zamani Abe, ambaye alistaafu mwaka wa 2020, alitembelea Nairobi mwaka wa 2016 wakati wa mkutano wa 6 wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD), ambapo alifanya mazungumzo na Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi.

Shinzo alifariki baada ya kupigwa risasi alipokuwa akitoa hotuba ya kampeni ya uchaguzi katika jiji la Nara, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.

Mtangazaji wa NHK na shirika la habari la Kyodo liliripoti kifo cha Abe siku ya Ijumaa, saa chache baada ya mzee huyo wa miaka 67 kupigwa risasi kifuani na shingoni.

Hata hivyo polisi walimkabili mshukiwa wa shambulizi dhidi ya Abe.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved