logo

NOW ON AIR

Listen in Live

TSC yawafuta kazi walimu 73 kutokana na makosa mbalimbali

"Endapo jina la mwalimu yeyote litaondolewa kwenye usajili chini ya Sheria hii, jina hilo halitarejeshwa isipokuwa kwa maelekezo ya Tume."

image
na

Habari20 July 2022 - 07:50

Muhtasari


•Kutokana na notisi hiyo, walimu hao wote waliondolewa kwenye orodha Juni 22, mwaka huu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Utumishi wa Walimu Nancy Macharia.

Baadhi ya walimu 73 hawataruhusiwa kutoa huduma zao katika taasisi yoyote ya mafunzo.

Haya ni kulingana na ilani ya Tume ya Kuajiri Walimu iliyochapisha orodha ya walimu 73 walioathiriwa.

"Kulingana na kifungu cha 30 cha Sheria ya TSC (2012), Tume inapendekeza  kuchapisha majina ya walimu ambao wameondolewa kwenye Rejista ya Walimu," notisi hiyo ilisema.

Kulingana na Sheria ya TSC, kuna sababu tano ambazo zinaweza kusababisha mwalimu kuondolewa kwenye sajili.

Baadhi ya sababu ni pamoja na; ikiwa mwalimu amekufa, Tume isiporidhika  jinsi mwalimu alipata usajili uenda ni kwa njia za udanganyifu na ikiwa mtu amepatikana kujihusishwa kimapenzi na mwanafunzi.

Kama wametiwa hatiani kwa kosa la jinai ambalo kwa maoni ya Tume linamfanya mtu huyo kuwa hafai kuwa mwalimu; (e) ambaye Tume imeagiza aondolewe kwa sababu ya taratibu za kinidhamu,” kipenge cha  Sheria hiyo.

“Iwapo watapatwa na maradhi hayo ya kimwili au kiakili au udhaifu ambao unamfanya mtu huyo kushindwa kutekeleza majukumu ya ualimu, kuondolewa,''

Sheria pia inaelekeza kuwa TSC itachapisha jina na maelezo ya mwalimu ndani ya mwezi mmoja baada ya kuondolewa

"Endapo jina la mwalimu yeyote litaondolewa kwenye usajili chini ya Sheria hii, jina hilo halitarejeshwa isipokuwa kwa maelekezo ya Tume."

Zaidi ya hayo, mwalimu ambaye jina lake limeondolewa kwenye sajili ya TSC atakoma kuhudumu kama mwalimu kuanzia tarehe ya kuondolewa.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved