logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watoto wapatikana wakisafirisha misokoto 347 ya bangi huku mimea 364 iking'olewa

NPS imewakumbusha raia kuwa matumizi ya mihadarati yanaharibu maisha na familia nyingi

image
na Radio Jambo

Habari21 July 2022 - 02:56

Muhtasari


•Polisi waling'oa mimea 364 ya bangi  katika shamba ya mshukiwa ambaye alitambulishwa kama Joseph Ng'ang'a.

•Polisi kutoka Siaya walipata misokoto 347 ya bangi ikiwa imefichwa kwenye suitcase na begi la safari.

Jamaa mmoja anasakwa na polisi kwa madai ya kupanda bangi katika shamba yake lililoko eneo la Solai, kaunti ya Nakuru.

Jumatano polisi kutoka kituo cha Solai kwa usaidizi wa utawala wa eneo hilo waling'oa mimea 364 ya mihadarati hiyo haramu nchini katika shamba ya mshukiwa ambaye alitambulishwa kama Joseph Ng'ang'a.

Maafisa hao hata hivyo hawakuweza kumtia mbaroni mshukiwa kwani alitoweka na hajulikani aliko hadi kufikia sasa.

Tume ya huduma kwa polisi imetangaza kupitia taarifa kuwa msako dhidi ya mshukiwa umeimarishwa.

Katika tukio tofauti, polisi kutoka kituo cha Unguja, kaunti ya Siaya  waliweza kupata misokoto 347 ya bangi ikiwa imefichwa kwenye suitcase na begi la safari la washukiwa ambao walikuwa wamepanga safari ya kwenda Nairobi.

Washukiwa ambao wanaaminika kuwa watoto wadogo waliacha mizigo yao na kutoweka walipohojiwa na wafanyikazi wa kampuni ya basi ambalo walikuwa wamepanga kuhusu walichokuwa wamebeba.

Polisi wametangaza kwamba uchunguzi unaendelea ili kuwatambua washukiwa na wenye mihadarati ile.

"Tume ya Huduma kwa Polisi, kupitia Idara ya Watoto na Jinsia kote nchini, daima imekuwa ikitetea haki na ustawi wa watoto. Tunawakumbusha umma, hasa wazazi, jukumu lao katika kuwalinda watoto dhidi ya aina yoyote ya ulanguzi na unyanyasaji wa dawa za kulevya kama inavyopendekezwa na Sheria ya Watoto Nambari. 8 ya 2001. Usafirishaji wa bangi ni kosa kubwa na huvutia adhabu kubwa," Taarifa ya NPS imesoma.

NPS pia imewakumbusha raia kuwa matumizi ya mihadarati yanaharibu maisha hasa ya vijana na kuwazuia kuishi maisha mazuri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved