logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raia wa Misri auawa mtaani Jamhuri alipoenda kudai pesa zake

Mshukiwa alichukua kisu na kumdunga mhasiriwa mara nane, mwenzake alidungwa pajani

image
na

Habari28 July 2022 - 07:42

Muhtasari


• Polisi waliitwa na jirani baada ya kusikia zogo na kupata watu watatu wakiwa na majeraha ya kudungwa kisu.

• Walikimbizwa katika hospitali ya Coptic ambapo Alsaid alifariki akipokea matibabu. Mwenzake alilazwa lakini hali yake ni thabiti.

Crime scene

Raia mmoja wa Misri ambaye alikuwa ameenda kudai  deni lake kutoka kwa jirani yake alifariki baada ya kudungwa kisu mara nane katika mapigano mtaa wa Jamhuri jijini Nairobi.

Marehemu aliyetambulika kama Ayman Alsaid inasemekana alidungwa kisu mara nane na mshukiwa aliyejaribu pia kujiua kwa kujikata koo.

Polisi walioitwa na jirani baada ya kusikia zogo katika ghorofa ya Orange mtaani Jamhuri walipata watu watatu wakiwa na majeraha ya kudungwa kisu.

Polisi walisema Alsaid na mwenzake alienda kwa nyumba ya mshukiwa na kutaka walipwe deni lao.

Kisha alikasirika na kwenda jikoni, akachukua kisu na kumchoma mhasiriwa mara nane huku mwenzake akichomwa kisu kwenye paja kabla ya kujigeuzia kisu hicho mwenyewe.

Watatu hao walikimbizwa katika hospitali ya Coptic ambapo Alsaid alifariki akipokea matibabu. Mwenzake alilazwa lakini hali yake ni thabiti.

Kwingineko,

Polisi wanasaka genge lililovamia nyumba moja eneo la Chumvi kwenye Barabara kuu ya Mombasa huko Machakos na kumuua mfanyikazi wa nyumbani wakati wa wizi huo.

Mfanyikazi huyo wa kike alikuwa peke yake ndani ya nyumba wakati genge hilo lilipovamia na kumnyonga kabla ya kutoroka na bidhaa za nyumbani zenye thamani ya maelfu ya pesa.

Polisi wanasema wamiliki wa nyumba hiyo walikuwa wamemwacha mwanamke huyo peke yake ndani ya nyumba wakati genge hilo lilipovamia Jumatano alasiri. Msako dhidi ya genge unaendelea.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved