logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Barabara ya Nairobi Expressway yafungwa

Hatua hii inafuatia mwisho wa kipindi cha majaribio ambacho madereva walikuwa wamepatiwa.

image
na Radio Jambo

Burudani31 July 2022 - 05:08

Muhtasari


•Kufungwa kwa expressway kunafuatia mwisho wa kipindi cha majaribio ambacho madereva walikuwa wamepatiwa.

•Awamu ya majaribio ilikuwa ni kutathmini mradi na kujua nini kifanyike ili kuwezesha utoaji wa huduma kwa ufanisi.

Barabara kuu ya Expressway jijini Nairobi, Kenya

Barabara ya Nairobi Expressway ilifungwa kwa waendesha magari kuanzia Jumamosi, Julai 30 mwendo wa saa tatu usiku.

Kampuni ya Moja Expressway inayosimamia barabara hiyo, ilisema hatua hiyo inafuatia mwisho wa kipindi cha majaribio ambacho walikuwa wamepatia madereva. 

Barabara hiyo inayounganisha upande wa Magharibi wa Nairobi na ule wa Mashariki itaanza kutumika tena mara tu itakapozinduliwa rasmi.

Kampuni hiyo ilisema madereva wataarifiwa na kushauriwa mara huduma zitakaporejea.

"Kipindi cha majaribio kwa Barabara ya Nairobi Expressway, kilichoanza Mei 14, 2022, kimefikia kikomo," Kampuni ya Moja Expressway ilisema katika taarifa.

"Barabara hiyo sasa itafungwa rasmi kuanzia saa tatu usiku Jumamosi, Julai 30, 2022 hadi itakapoanza kutumika rasmi. Kampuni ya Moja Expressway inasikitika kwa usumbufu uliojitokeza na madereva wa magari watapewa ushauri pindi watakaporejesha huduma kwenye barabara hiyo."

Awamu ya majaribio ilikuwa ni kutathmini mradi na kujua nini kifanyike ili kuwezesha utoaji wa huduma kwa ufanisi.

Katika awamu za majaribio, ajali kadhaa zimeripotiwa katika barabara hiyo, hasa katika kituo cha kulipia ada cha Mlolongo.

Matukio kama haya sasa yanaipa kampuni fursa ya kubuni njia za kuhakikisha kuwa barabara ni salama na madereva wa magari hufuata taratibu za kawaida za uendeshaji ili kuepusha visa vya kutisha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved