logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nyumba ya DPP Noordin Haji Nairobi Yavamiwa na Majambazi

Kulingana na ripoti ya polisi, idadi isiyojulikana ya majambazi walivamia makazi ya DPP na kuiba vifaa vya elektroniki.

image
na Radio Jambo

Habari05 August 2022 - 09:36

Muhtasari


•Polisi walifika eneo la tukio na kunakili chini vifaa vilivyoibiwa huku  wakisubiri kuanza  uchunguzi.

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji

Makao ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji katika kitongoji cha Riverside jijini Nairobi yalivunjwa usiku wa Alhamisi, Agosti 5, na watu wasiojulikana.

Kulingana na ripoti ya polisi, idadi isiyojulikana ya majambazi walivamia makazi ya DPP na kuiba vifaa vya elektroniki.

Moja wa vyombo vya habari humu nchini iliripoti kuwa wakati wa uvamizi huo, mfanyakazi wa nyumba wawili na watoto walikuwa ndani ya nyumba hiyo lakini hakuna aliyesikia chochote.

DPP Haji hakuwepo nyumbani wakati wa uvamizi huo.

Majambazi hao walitoweka na tarakilishi mbili, TV ya Samsung ya inchi 75, Sony PlayStation 4, viatu vya aina mbalimbali na mifuko miwili.

Polisi walifika eneo la tukio na kunakili chini vifaa vilivyoibiwa huku  wakisubiri kuanza  uchunguzi.

Huduma ya Polisi ya Kitaifa tangu wakati huo imeimarisha ulinzi katika makazi hayo hata kama wanawasaka majambazi.

Kufuatia wizi huo, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (ODPP) ilithibitisha kutokea kwa wizi huo. Hata hivyo, ilitupilia mbali taarifa kwamba ofisi hiyo pia ilivamiwa na majambazi hao.

“DPP angependa kufafanua kuwa kulikuwa na wizi kwenye makazi yake, si ofisi yake, na uchunguzi unaendelea.ODPP, kama Mamlaka ya Mashtaka, haisanyi au kuhifadhi ushahidi wa aina yoyote. Umma na vyombo vya habari wanahimizwa kutoingiza siasa kwenye tukio hili,"  Baadhi ya maneno kutoka taarifa hiyo ilesema.

Ijapokuwa usalama umeimarishwa katika maeneo mbalimbali nchini, idadi ya majambazi wanaovamia nyumba katika mashamba ya kifahari jijini Nairobi pia imeongezeka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved