logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DCI wamtaka Moses Kuria kuandika taarifa kuhusu madai ya wizi wa kura

Hii ni baada ya madai aliyoandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kuhusu njama ya kuiba kura.

image
na Radio Jambo

Habari08 August 2022 - 17:18

Muhtasari


  • Hii ni baada ya madai aliyoandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kuhusu njama ya kuiba kura

Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria ameatakiwa kufika mbele ya afisi za DCI haraka iwezekanavyo.

Hii ni baada ya madai aliyoandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kuhusu njama ya kuiba kura.

"DCI wamepata habari kuhusu chapisho la kuzua joto ambazlo linahusishwa na Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kurua akizungumzia madai mazito kuhusu kosa linalohusu uchaguzi," DCI ilisema.

Walisema anafaa kufika katika afisi yoyote ya DCI iliyo karibu naye ili kuandika taarifa zaidi kuhusu anayoyajua.

"DCI inamtaka mbunge huyo kuripoti kwa haraka katika kituo cha polisi au afisi za DCI zilizo karibu naye ili kuwezesha uchunguzi kufanywa na hatua kuchukuliwa. Taarifa kamili itasaidia pakubwa katika kuhakikisha kuwa hatua imechukuliwa," taarifa ya DCI iliongeza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved