logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kwa Mungu yote yanawezekana-Ruto asema baada ya uamuzi wa mahakama

Ruto alipata 7.1m huku Raila Odinga akipata 6.9m kama ilivyotangazwa na IEBC.

image
na Radio Jambo

Habari05 September 2022 - 12:13

Muhtasari


  • Katika taarifa yake baada ya Mahakama ya upeo kuidhinisha uchaguzi wake wa urais, Ruto alisema safari yake ya kuwa rais ni ushahidi wa mapenzi ya Mungu

Rais mteule William Ruto bado amehusisha ushindi wake na Mungu.

Katika taarifa yake baada ya Mahakama ya upeo kuidhinisha uchaguzi wake wa urais, Ruto alisema safari yake ya kuwa rais ni ushahidi wa mapenzi ya Mungu.

"Kwa wanadamu haiwezekani, lakini si kwa Mungu: kwa maana kwa Mungu yote yanawezekana," aliandika.

Mahakama ya upeo ya Kenya Jumatatu ilithibitisha kuchaguliwa kwa William Ruto kama Rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya.

Akisoma uamuzi wa Mahakama yaupeo Jumatatu, Jaji Mkuu Martha Koome alisema Ruto alipata asilimia 50 pamoja na kura moja iliyohitajika ili mmoja atangazwe mshindi.

Mnamo Agosti 15, mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alimtangaza Ruto kuwa Rais mteule baada ya kuwashinda Raila na wagombeaji wengine wawili katika uchaguzi wa Agosti 9.

Ruto alipata 7.1m huku Raila Odinga akipata 6.9m kama ilivyotangazwa na IEBC.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved