logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtaala wa CBC hautakomeshwa, DP Gachagua asema

DP pia alichukua fursa hiyo kuwaomba Wakenya kushiriki katika mchakato huo mara tu utakapoanza.

image
na Radio Jambo

Habari23 September 2022 - 17:14

Muhtasari


  • Alibainisha zaidi kwamba serikali imejitolea kwa uchumi wa ubunifu na maendeleo ya vijana kuwa viongozi wa kesho
Naibu rais mteule Rigathi Gachagua

Naibu Rais Gachagua Rigathi amesema serikali haitabatilisha Mtaala Unaozingatia Umahiri.

Gachagua alisema badala yake wanaipitia ili waweze kuhifadhi yale yaliyo mema na kuyaboresha.

Alisema kumekuwa na mashaka kutoka kwa walimu, wazazi na wadau wengine kwenye CBC na hivyo kutaka kuangaliwa upya.

“Serikali yetu hivi karibuni itazindua kikosi kazi kitakachoangalia mageuzi ya kielimu ikiwamo CBC kwa nia ya kuipitia na si kuifuta,” alisema.

Alizungumza wakati wa kufungwa kwa Tamasha la 94 la Muziki la Kenya katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Kisumu.

DP pia alichukua fursa hiyo kuwaomba Wakenya kushiriki katika mchakato huo mara tu utakapoanza.

“Msilalamike tu kwenye nyumba zenu au sokoni, vituoni, jitokezeni kwa wingi na toeni maoni yenu kuhusu kile mnachotaka kiboreshwe,” alisema.

Alibainisha zaidi kwamba serikali imejitolea kwa uchumi wa ubunifu na maendeleo ya vijana kuwa viongozi wa kesho.

“Serikali yetu imejizatiti kutoa sera na mipango madhubuti ili kuhakikisha kuwa vipaji vya vijana wetu vinatafsiriwa kuwa chanzo cha mapato kwao,” alisema. 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved