logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila ataka Interpol kuongoza uchunguzi wa kifo cha wakili Paul Gicheru

Raila alitaja kifo hicho kuwa cha kushangaza na kisichoelezeka.

image
na Radio Jambo

Habari29 September 2022 - 05:15

Muhtasari


• Waziri Mkuu huyo wa zamani aliifariji familia ya Gicheru na kutaka uchunguzi ufanyike kuhusu ugonjwa wa mwana wao.

Kiongozi wa Azimio Raila Odinga amewataka polisi wa Kimataifa wa Interpol kuanzisha uchunguzi kuhusiana na kifo cha mshukiwa wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), wakili Paul Gicheru.

Katika taarifa iliotolewa na msemaji wa Raila Prof Makau Mutua mnamo Jumatano, Septemba 28, Raila alitaja kifo hicho kuwa cha kushangaza na kisichoelezeka.

"Mfano wa vifo vya ajabu na visivyoelezeka, vingine vikiwa vya kutisha na vibaya, ni vya kutatanisha sana.

Amesema kwamba ili kuzuia mauaji hayo kuzimwa, amewataka maafisa wa Interpol kuongoza Uchunguzi huo, ilisema Taarifa hiyo.

Raila alieleza kuwa kifo cha Gicheru kilikuwa na athari za kimataifa kwani ICC ilimweka kizuizini wakati wa kifo chake.

Alisema kuwa kwasababu ya kuwa mwanachama wa Mahakama hiyo yenye makao yake The Hague, Kenya haikuwa na chaguo ila kuruhusu uchunguzi.

Waziri Mkuu huyo wa zamani aliifariji familia ya Gicheru na kutaka uchunguzi ufanyike kuhusu ugonjwa wa mwana wao.

Gicheru alikuwa ameshtakiwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu kwa kuingilia mashahidi kuhusiana na kesi ya ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007-08, ambapo alikana mashtaka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved