logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pigo kwa rais William Ruto, kamati ya uteuzi yakataa uteuzi wa Malonza kuwa waziri wa utalii

Kamati hiyo pia iliidhinisha uteuzi wa Justin Muturi kama Mwanasheria Mkuu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri25 October 2022 - 12:09

Muhtasari


• Kamati inayoongozwa na Spika Moses Wetang'ula iliidhinisha uteuzi wa wateule wengine 21 wa Baraza la Mawaziri.

• Kiranja wa walio wachache Junet Mohamed, hata hivyo, alisema upande wa wachache umeandika ripoti yao kukataa uteuzi wa Aisha Jumwa na Mithika Linturi. 

Peninah Malonza aliyependekezwa kuwa waziri la Utalii, Wanyamapori na Turathi wakati wa akihojiwa na Kamati ya Bunge kuhusu uteuzi Oktoba 19, 2022. Picha: EZEKIEL AMING'A

Kamati ya Bunge ya Uteuzi imekataa kwa kauli moja pendekezo la rais William Ruto kumteua Peninah Malonza kuwa waziri wa Utalii, Wanyamapori na Turathi za kitaifa.

Katika notisi ya hoja hiyo, Kiongozi wa Wengi Kimani Ichungwah alisema Kamati inayoongozwa na Spika Moses Wetang'ula iliidhinisha uteuzi wa wateule wengine 21 wa Baraza la Mawaziri.

Kamati hiyo pia iliidhinisha uteuzi wa Justin Muturi kama Mwanasheria Mkuu na Mercy Wanjau kama Katibu wa Baraza la Mawaziri.

Kiranja wa walio wachache Junet Mohamed, hata hivyo, alisema upande wa wachache umeandika ripoti yao kukataa uteuzi wa Aisha Jumwa na Mithika Linturi. 

Rais William Ruto alimpendekeza Jumwa kuwa waziri wa Utumishi wa Umma na Jinsia na Linturi kwa wizara ya Kilimo na ustawi wa Mifugo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved