logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kenya kupeleka vikosi vyake DRC kupambana na makundi yenye silaha

Vikosi vya Kenya vitajiunga na kikosi cha kanda kitakachosaidia kupambana na makundi yenye silaha.

image
na Samuel Maina

Habari02 November 2022 - 03:44

Muhtasari


  • •Rais William Ruto ataongoza shughuli ya kuaga kikosi cha Jeshi la Ulinzi la Kenya - KDF kinachoelekea Mashariki mwa DRC.

Rais William Ruto ataongoza shughuli ya kuaga kikosi cha Jeshi la Ulinzi la Kenya - KDF kinachoelekea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo - DRC ambapo mapigano makali yanaendelea kati ya jeshi na wanamgambo wa M23.

Jeshi la DRC pia linajishughulisha na pande nyingine zinazopigana na kundi la Islamic State - Allied Democratic Forces ADF, na makundi mengine kadhaa yenye silaha.

Vikosi vya Kenya vitajiunga na kikosi cha kanda kitakachosaidia kupambana na makundi yenye silaha.

Wazo la kutuma jeshi la kikanda lilitolewa na kuidhinishwa mwezi Juni, wakati Rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta (sasa mjumbe wa amani wa Kenya) alipoitisha mkutano wa amani (Mchakato wa Nairobi) wa viongozi wa EAC.

Kenya ilichaguliwa kuongoza juhudi za kidiplomasia na kijeshi.

Hii ni mara ya kwanza kwa EAC kutuma wanajeshi katika nchi wanachama. Itakuwa mtihani mdogo wa uwezo wa kambi hiyo kushughulikia changamoto tata za kisiasa na usalama.

Kikosi cha Kenya ambacho kilipelekwa mwaka jana kujiunga na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC - MONUSC kwa mwaliko wa Rais Felix Tshisekedi tangu wakati huo kiondolewa na kurejeshwa nyumbani Kenya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved