logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Natembeya akutana na muuguzi aliyemchezea densi mtoto mgonjwa

Hongera Elizabeth Robai juhudi na kujitolea kwako vimezaa matunda,"Natembeya Alisema.

image
na Radio Jambo

Habari08 November 2022 - 18:43

Muhtasari


  • Natembeya alimkaribisha Elizabeth Robai Lukelesia Jumanne jioni katika ofisi yake katika makao makuu ya kaunti ya Trans Nzoia ili kumshukuru rasmi kwa ishara yake

Gavana wa Trans Nzoia George Natembeya amemsifu muuguzi wa Chuo cha Mafunzo ya Udaktari cha Kenya (KMTC) ambaye amevumaa mitandaoni kwa kumtumbuiza mtoto mgonjwa katika wadi.

Natembeya alimkaribisha Elizabeth Robai Lukelesia Jumanne jioni katika ofisi yake katika makao makuu ya kaunti ya Trans Nzoia ili kumshukuru rasmi kwa ishara yake.

"Niliweza kukutana na muuguzi wa watoto Robai Elizabeth Lukelesia jioni hii. Muuguzi aliyejitolea anayehudumu kwa bidii."

Natembeya aliahidi kumlipia ada ya shule mwanafunzi huyo.

"Nimeahidi kumlipia ada ya masomo kwa muda uliosalia wa masomo yake, zaidi kuhakikisha anapata mafunzo ya kazi na hatimaye kufyonzwa ili kuhudumu kama muuguzi wa watoto.

Hongera Elizabeth Robai juhudi na kujitolea kwako vimezaa matunda,"Natembeya Alisema.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved