logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shule kufungwa kwa miezi 2 huku mitihani ya kitaifa iking'oa nanga wiki kesho

Shule zinatarajiwa kufungwa Novemba 24 na kufunguliwa mwaka ujao Januari 23, 2023.

image
na Radio Jambo

Habari23 November 2022 - 12:19

Muhtasari


• Watahiniwa wa gredi ya 6 na darasa la nane  wataanza mitihani yao Novemba 28.

• Wanafuzi wa kidato cha nne wataanza KCSE mnamo Desemba 02, 2022.

Ratiba ya kalenda ya masomo mwaka wa 2023 Kenya

Wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari zinafungwa rasmi Ijumaa Novemba 25 kwa likizo ndefu ya wiki nane.

Wanafunzi wanatarajiwa kufunga shule hili kuwapa nafasi watahiniwa wa mitihani ya kitaifa kufanya mtihani wao  wa CBC wa gredi ya 6, KCPE wa darasa la nane, na KCSE kwa wanafunzi wa kidato cha 4 unaotarajiwa kuanza wiki ijayo.

Wanafunzi wa gredi ya 6 na darasa la nane  wanataanza mtihani wao mnamo Novemba 28 hadi Novemba 30.

Watahiniwa wa kidato cha nne wanatarajiwa kuanza  siku ya Alhamisi Desemba 02, 2022 na kumaliza tarehe 23 Desemba 2022.

Mbali na hayo wazazi wamelilia kuongezeka kwa karo ya shule ambayo ni pigo kubwa kwao kwani ni mzigo mkubwa kwao.

Haya yamejiri baada ya  serikali kuondoa ruzuku iliyokuwa inawasaidia wazazi kulipa karo kidogo ila sasa ni pigo kwa wazazi maana karo itapanda kwanzia mwaka ujao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved