Shule kufungwa kwa miezi 2 huku mitihani ya kitaifa iking'oa nanga wiki kesho

Shule zitagungwa kwanzia Novemba 24 kwa likozi ndefu ya wiki 8.

Muhtasari

• Watahiniwa wa gredi ya 6 na darasa la nane  wataanza mitihani yao Novemba 28.

• Wanafuzi wa kidato cha nne wataanza KCSE mnamo Desemba 02, 2022.

Ratiba ya kalenda ya masomo mwaka wa 2023 Kenya
Radio Jambo Ratiba ya kalenda ya masomo mwaka wa 2023 Kenya
Image: Hillary Bett

Wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari zinafungwa rasmi Ijumaa Novemba 25 kwa likizo ndefu ya wiki nane.

Wanafunzi wanatarajiwa kufunga shule hili kuwapa nafasi watahiniwa wa mitihani ya kitaifa kufanya mtihani wao  wa CBC wa gredi ya 6, KCPE wa darasa la nane, na KCSE kwa wanafunzi wa kidato cha 4 unaotarajiwa kuanza wiki ijayo.

Wanafunzi wa gredi ya 6 na darasa la nane  wanataanza mtihani wao mnamo Novemba 28 hadi Novemba 30.

Watahiniwa wa kidato cha nne wanatarajiwa kuanza  siku ya Alhamisi Desemba 02, 2022 na kumaliza tarehe 23 Desemba 2022.

Mbali na hayo wazazi wamelilia kuongezeka kwa karo ya shule ambayo ni pigo kubwa kwao kwani ni mzigo mkubwa kwao.

Haya yamejiri baada ya  serikali kuondoa ruzuku iliyokuwa inawasaidia wazazi kulipa karo kidogo ila sasa ni pigo kwa wazazi maana karo itapanda kwanzia mwaka ujao.