logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi hawakutumia vitoa machozi wakati wa uchaguzi wa Agosti - Mkuu wa polisi

Lamet alisema Huduma ya Kitaifa ya Polisi itaendelea kuimarisha ushirikiano wa karibu na IEBC

image
na Radio Jambo

Habari16 January 2023 - 09:59

Muhtasari


  • Lamet alisema mafunzo ya maafisa wa polisi waliosimamia uchaguzi huo yalichangia utulivu ulioshuhudiwa wakati wa uchaguzi

Inspekta Jenerali Msaidizi wa Polisi Judy Lamet amefichua kuwa Polisi hawakufyatua risasi moja au kurusha vitoa machozi kwa mtu yeyote wakati wa uchaguzi wa Agosti 9 2022.

Lamet alisema mafunzo ya maafisa wa polisi waliosimamia uchaguzi huo yalichangia utulivu ulioshuhudiwa wakati wa uchaguzi.

"Mafunzo mengi yalifanyika kuanzia kada ya chini hadi juu. Mafunzo haya yalifanyika na wadau wengine," alisema.

Lamet alikuwa akizungumza katika Hoteli ya Safari Park Jumatatu wakati wa uzinduzi wa ripoti ya IEBC ya tathmini ya baada ya uchaguzi wa Agosti 9, 2022.

Lamet alibainisha zaidi kwamba maafisa kutoka magereza na Huduma ya Kitaifa ya Vijana ambao walihusika katika uchaguzi pia walipewa mafunzo.

"Pia walipata mafunzo kwa sababu walilinda kura, vituo vya kupigia kura na hata kituo cha kitaifa cha kuhesabu kura," aliongeza.

"Pia nataka kuwashukuru washikadau ambao walitoa huduma zingine kama vile miongozo ya usalama wa uchaguzi kwa maafisa wetu."

Lamet alisema Huduma ya Kitaifa ya Polisi itaendelea kuimarisha ushirikiano wa karibu na IEBC na washikadau wanaohusika katika usimamizi wa uchaguzi.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved