logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nyamu apewa muda zaidi na kamati ya nidhamu ya UDA kujibu mashtaka dhidi yake

Mashtaka dhidi ya seneta yanahusu mwenendo wake 'wa aibu' mnamo Desemba 16, 2022

image
na Radio Jambo

Habari20 January 2023 - 14:00

Muhtasari


  • Baadhi ya Wakenya walitaka afukuzwe katika chama na kusema kuwa amekiuka Sura ya Sita ya Katiba kuhusu Uongozi na Uadilifu
Nyamu asema haachi pombe

Seneta mteule Karen Nyamu amepewa muda zaidi na kamati ya nidhamu ya UDA kujibu tuhuma dhidi yake.

Alifika mbele ya kamati hiyo siku ya Ijumaa ambapo kikao hicho kiliahirishwa hadi Februari 24 saa tatu asubuhi.

"Seneta aliruhusiwa muda zaidi kujibu tuhuma zilizotolewa dhidi yake na mwanachama wa chama," chama cha United Democratic kilisema kwenye notisi.

Mashtaka dhidi ya seneta yanahusu mwenendo wake 'wa aibu' mnamo Desemba 16, 2022

Mbunge huyo alizua taharuki katika tamasha la msanii wa Mugithi Samidoh mjini Dubai na kusababisha mzozo na mkewe Edday Nderitu.

Katika kipande cha video ambacho kilisambaa mtandaoni, Nyamu alionekana akizuiliwa na walinzi wa tukio hilo wakati wa tamasha hilo.

Klipu tofauti ilionyesha Nyamu akicheza dansi jukwaani huku mwimbaji Samidoh na Karangu Muraya wakitumbuiza washereheshaji muda mfupi kabla ya kuondolewa baada ya ugomvi.

Seneta huyo baadaye alilaumu pombe kwa ajili ya matendo yake , tabia ambayo aliapa kuacha Januari mwaka huu.

Baadhi ya Wakenya walitaka afukuzwe katika chama na kusema kuwa amekiuka Sura ya Sita ya Katiba kuhusu Uongozi na Uadilifu.

Aliyekuwa mgombea urais wa UDA Japhnei Orina alikuwa miongoni mwa waliotoa wito kwa chama hicho kuanza mchakato wa kumtimua.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved