logo

NOW ON AIR

Listen in Live

NSAC ilitaka Raila Odinga atangazwe mshindi-Guliye

"Tulipokaribia kumaliza, mwenyekiti aliitisha mkutano saa 2 jioni na huu ulikuwa mkutano wa makamishna

image
na Radio Jambo

Habari23 January 2023 - 10:10

Muhtasari


  • Kulingana na hati ya kiapo ya Guliye, mwenyekiti wa wakati huo Wafula Chebukati alikubali wito huo lakini alilazimika kuahirisha mkutano huo hadi saa 2:00 adhuhuri

Aliyekuwa kamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Abdi Guliye sasa anadai kuwa saa chache kabla ya kutangaza matokeo ya urais wa Agosti 2022, waliambiwa wamtangaze kiongozi wa Azimio la Umoja Raila Odinga kuwa mshindi  wa uchaguzi huo.

Guliye alitoa ushahidi mbele ya kamati ya uchunguzi wa uchaguzi inayoongozwa na Jaji Aggrey Muchelule Jumatatu akisema kwamba mnamo Agosti 15, 2022, saa chache kabla ya kutangaza matokeo ya mwisho ya urais, timu ya wageni wanne walidai kuhudhuria kikao pamoja na makamishna wote mwendo wa saa nne asubuhi.

Kulingana na hati ya kiapo ya Guliye, mwenyekiti wa wakati huo Wafula Chebukati alikubali wito huo lakini alilazimika kuahirisha mkutano huo hadi saa nane alasiri kwa sababu alikuwa anakamilisha baadhi ya michakato ya uhakiki wa kura.

“Walitaka kumuona mwenyekiti na akasema tutaonana lakini alikuwa anamalizia kwanza baadhi ya taratibu za uhakiki na tutawaona saa mbili kamili,” alibainisha.

Guliye aliendelea kusema kuwa katika muda uliopangwa upya, Chebukati aliwaita wote, wakiwemo wageni hao wanne, kwenye chumba cha mikutano cha Mkurugenzi Mtendaji wa Bomas.

"Tulipokaribia kumaliza, mwenyekiti aliitisha mkutano saa 2 jioni na huu ulikuwa mkutano wa makamishna na matarajio yetu yalikuwa kwamba matokeo ya mwisho yangechapishwa,"alisema.

Guliye alisema kuwa timu hiyo ya watu wanne ilitambulishwa, na wakasema kwamba walikuwa hapo kwa niaba ya Kamati ya Ushauri ya Usalama wa Kitaifa (NSAC).


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved