logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tukutane Kamukunji-Raila asema baada ya kurejea nchini

Nimefurahi kurejea nyumbani, tukutane Kamukunji," Raila alisema.

image
na Radio Jambo

Makala23 January 2023 - 10:39

Muhtasari


  • Waziri Mkuu huyo wa zamani alikuwa ametangaza kwamba atafanya mazungumzo ya umma katika uwanja wa Kamukunji, Nairobi, muda mfupi baada ya kutua nchini

Kiongozi wa Chama cha Azimio alirejea Nchini Jumatatu, Januari 23, kutoka kwa safari ya kikazi nchini Afrika Kusini.

Odinga alipokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA), na wakuu wa Azimio, akiwemo Martha Karua na Kalonzo Musyoka.

Wengine katika uwanja huo wa ndege ni aliyekuwa Katibu wa Baraza la Mawaziri Eugene Wamalwa, msemaji wa Chama cha Azimio Makau Mutua,Jeremiah Kioni,Wycliffe Oparanya miongoni mwa viongozi wengine.

Nimefurahi kurejea nyumbani, tukutane Kamukunji," Raila alisema.

Waziri Mkuu huyo wa zamani alikuwa ametangaza kwamba atafanya mazungumzo ya umma katika uwanja wa Kamukunji, Nairobi, muda mfupi baada ya kutua nchini.

Mkutano huo ulipangwa baada ya mdokezi kudai kwamba alikuwa na ushahidi wa wizi mkubwa uliotokea katika Mlima Kenya wakati wa  uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved