logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Machogu aamuru kurejeshwa kazini kwa VC wa chuo cha Meru baada ya wanafunzi kuandamana

Machogu alitaja hatua ya kusimamishwa kazi kwa Odhiambo kama isiyoeleweka.

image
na Radio Jambo

Habari07 March 2023 - 09:07

Muhtasari


•Machogu ameamuru kurejeshwa kazini kwa VC Romanus Odhiambo wa Chuo Kikuu cha Meru ambaye alifurushwa.

Waziri wa Elimu Ezekiel Machogu ameamuru kurejeshwa kazini kwa VC Romanus Odhiambo wa Chuo Kikuu cha Meru ambaye alifurushwa.

Katika taarifa yake ya Jumatatu, Machogu alitaja hatua ya kusimamishwa kazi kwa Odhiambo kama isiyoeleweka.

Hatua hiyo pia ilisababisha wanafunzi kufanya maandamano yaliyopelekea shule hiyo kufungwa Jumatatu.

"Wizara inaagiza baraza la chuo kikuu kubatilisha uamuzi wa kumtuma Odhiambo likizo ya mwisho na kumteua kaimu VC," Machogu alisema.

"Baraza la chuo kikuu limeagizwa kuwezesha kurejeshwa kwa Odhiambo kama VC mara moja, kwa vyovyote vile kabla ya kufungwa kwa biashara mnamo Machi 7."

Baraza lilisema halijashawishika kuwa VC huyo wa zamani alistahili muhula wa pili.

“Baraza la chuo kikuu katika kikao chake kilichofanyika Februari 27, 2023, lilitathmini utendaji wako na kubaini kuwa ulikuwa chini ya matarajio. Kwa hivyo, baraza lilikataa kufanya upya kandarasi yako kama ilivyoombwa katika barua yako ya tarehe 20 Desemba 2022,” mwenyekiti Prof Bosire Mwebi alisema katika barua ya Februari 27, 2023.

Siku ya Jumatatu wanafunzi walidai uamuzi wa baraza la chuo kikuu ulichochewa kisiasa na walitaka VC arejeshwe kazini mara moja.

Rais wa muungano wa wanafunzi Kariuki Wachira, akiungwa mkono na mtangulizi wake Hunnington Oguk, aliwaongoza wanafunzi katika maandamano na kuwashirikisha polisi katika mbio Jumatatu asubuhi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved