logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afisa wa polisi aliyejeruhiwa wakati wa maandamano Kisumu afariki

Alikuwa katika hospitali ya Aga Khan ambapo alifariki Alhamisi usiku akiwa ICU.

image
na

Yanayojiri31 March 2023 - 10:20

Muhtasari


• Baada ya polisi kuzidiwa nguvu, waandamanaji walivamia Jamia Supermarket na kuharibu na kuiba bidhaa dukani.

Jamia Supermarket ambapo afisa wa polisi Ben Oduor alijeruhiwa na waandamanaji siku ya Alhamisi, Machi 30. Picha: FAITH MATETE

Afisa wa polisi aliyeruhiwa wakati wa maandamano ya Muungano wa Azimio katika kaunti ya Kisumu amefariki.

Kulingana na ripoti ya polisi, afisa Ben Oduor wa kituo cha polisi cha Keroka huko Nyamira ambaye alikuwa akishika doria wakati wa maandamano mjini Kisumu alijeruhiwa katika eneo la Jamia Supermarket.

Afisa huyo akiwa ameandamana na wengine walizidiwa nguvu na waandamanaji waliokuwa wamezua ghasia.

Alikimbizwa kwa matibabu katika hospitali ya Aga Khan ambapo alifariki Alhamisi usiku akiwa katika chumba cha ICU.

Mwili wake unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ukisubiri uchunguzi wa maiti.

Wakati wa kisa cha Alhamisi baada ya maafisa hao kuzidiwa nguvu, waandamanaji walivamia duka hilo kuu, kuharibu na kuiba bidhaa dukani.

Mmiliki wa duka hilo Hussein Hassan alikuwa na machungu akihoji alichokuwa amewafanyia waandamanaji kiasi cha kudhalilishwa hivyo.

Hassan alisema alipoteza bidhaa zenye thamani ya mamilioni ya shilingi.

"Nina familia na watu wanaonitegemea na sijui nianzie wapi," alisikika akisema.

TAFSIRI: DAVIS OJIAMBO.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved