logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wezi wenye sare za polisi wavamia kituo cha mafuta Machakos

Walikuwa wamevalia mavazi yanayofanana na ya maafisa wa polisi.

image
na Radio Jambo

Habari22 April 2023 - 17:58

Muhtasari


  • Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Matungulu Peter Omondi alisema kisa hicho kilitokea mwendo wa saa 3.00 asubuhi Ijumaa.

Polisi wanawasaka wanaume saba ambao walinaswa kwenye CCTV wakati wa wizi ulioshindikana katika kituo cha mafuta cha Matungulu, Machakos.

Kanda ya CCTV iliyoonekana na Radiojambo inaonyesha watano kati ya wanaume waliovamia kituo cha mafuta kilichoko kando ya barabara ya Nairobi-Kangundo katika mji wa Tala.

Walikuwa wamevalia mavazi yanayofanana na ya maafisa wa polisi.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Matungulu Peter Omondi alisema kisa hicho kilitokea mwendo wa saa 3.00 asubuhi Ijumaa.

Picha za CCTV zinaonyesha watu hao wakipora ofisi ndani ya kituo cha mafuta saa 2:09:06 asubuhi.

Omondi alisema majambazi hao walijaribu kuiba kwenye kituo cha kujaza mafuta baada ya kuwavamia na kuwafunga wafanyakazi wake wawili na kuwafungia dukani bila mafanikio.

"Hili lilikuwa jaribio la wizi katika kituo cha mafuta cha Delta ambapo majambazi saba walivamia kituo hicho cha mafuta na kuwafunga wafanyikazi na kuwafungia dukani," Omondi aliambia Star Jumamosi.

"Baadaye walianza kuvunja chumba cha usalama lakini hawakuweza kwani polisi walitaarifiwa na mhudumu wa bodaboda."

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved