KFC yakanusha kuiba wazo la vyakula vya nchini Afrika Kusini

Muhtasari
  • Bw Malepe aliambia chapisho la eneo hilo kwamba wazo lake la "Streetwise Kota" liliibiwa alipokuwa akitafuta ushirikiano na KFC.
KFC Lyric House Mtaa wa Kimathi.
KFC Lyric House Mtaa wa Kimathi.
Image: FILE

Kampuni kubwa ya vyakula-KFC imekanusha madai ya mjasiriamali kutoka Afrika Kusini akiishutumu kampuni hiyo kwa kuiba wazo lake la chakula cha kienyeji kinachojulikana kama kota, zinasema ripoti za vyombo vya habari nchini humo.

Romeo Malepe anashutumu KFC kwa kutumia wazo lake la kota ya kuku ambayo KFC inazindua .

Kota, inayojulikana pia kama Sphatlo, ni sandwichi kubwa iliyo na viambato vingi vilivyowekwa ndani ya robo ya mkate, imefungwa na inaweza kuliwa ukiwa njiani.

Bw Malepe aliambia chapisho la eneo hilo kwamba wazo lake la "Streetwise Kota" liliibiwa alipokuwa akitafuta ushirikiano na KFC.

Bw Malepe pia anasemekana kujitokeza kwenye mitandao ya kijamii hivi majuzi kulaani KFC kwa madai ya kuchukua wazo lake ambalo alisema alilitengeneza miaka minne iliyopita.

Lakini KFC imekanusha madai hayo katika taarifa kwa vyombo vya habari vya Afrika Kusini, akisema kuwa "sio siri kwamba kota ni mlo maarufu wa Afrika Kusini na toleo dogo la KFC Sphatlho ni matokeo ya mchakato wa ndani wa kutengeneza bidhaa".

Ilisema kuwa kwa zaidi ya miaka 50, msururu huo umechochewa na turathi na utamaduni wa Afrika Kusini kuendeleza bidhaa za kibunifu za ndani katika orodha yao.

"Tutaendelea kutumia mitindo ya vyakula ya Afrika Kusini kama msukumo wa kuleta bidhaa muhimu kwa mashabiki wetu kote Afrika Kusini," KFC ilinukuliwa ikisema.