logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Upande wa mashtaka waomba Mackenzie aendelee kukaa kizuizini kwa siku 60 zaidi

"Kurudishwa rumande kwa muda wa siku 60 ni muda mdogo zaidi

image
na Radio Jambo

Habari02 June 2023 - 10:14

Muhtasari


  • Katika ombi la kutaka kuongezewa muda, upande wa mashtaka unasema  bado haujahitimisha uchunguzi na wanahitaji muda zaidi.

Pasta wa kanisa la Good News International Paul Mackenzie amefikishwa katika Mahakama ya Shanzu jijini Mombasa leo Ijumaa, Juni 2, 2023. ambapo upande wa mashtaka unaomba aendelee kuzuiliwa kwa siku 60 zaidi.

Katika ombi la kutaka kuongezewa muda, upande wa mashtaka unasema  bado haujahitimisha uchunguzi na wanahitaji muda zaidi.

"Kurudishwa rumande kwa muda wa siku 60 ni muda mdogo zaidi unaowezekana ambao upelelezi unaweza kukamilika chini ya mazingira yaliyopo na ni njia ndogo zaidi za kudumisha Uadilifu wa upelelezi dhaifu," zinasoma karatasi za mahakama.

Wanadai kuwa hakuna mabadiliko ya hali ya kuachiliwa huru kwa Mackenzie na washukiwa wengine 17 tangu uamuzi wa mahakama hiyo Mei 10 waliporudishwa rumande.

"Bado kuna sababu za msingi za kuwanyima dhamana hadi upelelezi ukamilike na kuna uwezekano mkubwa wa mashtaka makubwa dhidi ya washukiwa," zinasoma hati za mahakama.

Kufikia sasa miili ya watu zaidi ya 243 imeshafanyiwa upasuaji katika mochari ya Hospitali Kuu ya Malindi katika Kaunti ya Kilifi.

Wengi ni wale ambao miili yao iliondolewa kwenye makaburi ambayo maafisa wa usalama walipata msituni Shakahola.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved