Wito wa Maaskofu: Maaskofu wakatoliki wamtaka Ruto kufuta sheria ya fedha

Viongozi hao wamewataka viongozi wa pande mbili kusikiliza na kuzingatia maslahi ya wananchi

Muhtasari
  • Aidha wamewataka polisi kulinda usalama wa raia badala ya kutumia nguvu kupita kiasi na kusababisha vifo dhidi ya raia.
  • Viongozi hao pia walitangaza mipango ya kuitisha mazungumzo ya kitaifa huku wakiwataka Wakenya kupinga uchochezi na kuchochewa vurugu.
Maaskofu wakatoliki wamtaka Ruto kufuta sheria ya fedha
Image: DOUGLAS OKIDDY

Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya (KCCB) wanataka kufutwa kwa Sheria ya Fedha ya 2023 na kusitishwa kwa maandamano ya upinzani ambao wanasema umeiingiza nchi kwenye njia ya uharibifu.

Makasisi hao wanatoa changamoto kwa Rais William Ruto na kiongozi wa Azimio la Umoja One wa Kenya Raila Odinga kufikiria upya msimamo wao mkali na kukumbatia mazungumzo kama sehemu ya juhudi za kutafuta suluhu la kudumu kwa masuala yanayoisumbua nchi.

Viongozi hao wamewataka viongozi wa pande mbili kusikiliza na kuzingatia maslahi ya wananchi na kuhakikisha amani inapatikana kwa njia ya amani.

Aidha wamewataka polisi kulinda usalama wa raia badala ya kutumia nguvu kupita kiasi na kusababisha vifo dhidi ya raia.

Viongozi hao pia walitangaza mipango ya kuitisha mazungumzo ya kitaifa huku wakiwataka Wakenya kupinga uchochezi na kuchochewa vurugu.

Maaskofu wa Kanisa Katoliki wanasema wamejaribu bila mafanikio kuwafikia Rais William Ruto na kiongozi wa upinzani Raila Odinga ili kuweza kufanya mazungumzo nao huku maandamano ya kuipinga yakiendelea.

Akihutubia wanahabari jijini Nairobi siku ya Jumatano, mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya (KCCB) Askofu Mkuu Martin Kivuva alisema wako tayari kuwashirikisha viongozi hao wawili ili kupata suluhu la kirafiki ambalo litakomesha maandamano hayo.

“Tumejaribu kuwafikia wote wawili lakini hatujafanikiwa kuwaona ana kwa ana kwa sababu ya shughuli za wiki hii. Lakini wakisema wako tayari wiki hii tutakuwepo,” Askofu Mkuu Kivuva alisema.

Muungano wa Bw Odinga uliitisha maandamano hayo ili kupinga gharama ya juu ya maisha na kuongeza ushuru kwa utawala wa Ruto.

Maandamananoya awamu ya tatu yameanza tena siku ya Jumatano na upinzani unapanga kuyafanya kwa siku tatu kwa wiki . Upinzani ulirejea mtaani baada ya mazungumzo ya pande mbili kati ya wabunge wa upinzani na wenzao kushindikana, huku pande zote mbili zikilaumiana kwa kuhujumu mazungumzo.

Maaskofu hao wametoa wito wa kuanzishwa tena kwa mazungumzo hayo, safari hii yakihusisha viongozi wa makanisa. Walisema Wakenya wanapaswa kutumia njia zisizo za amani mahitaji yao.

“Wakenya na viongozi wetu lazima wawe tayari kusikilizana kwa ajili ya nchi yetu. Tunataka mazungumzo ya pande mbili ambayo hayakufaulu yarudishwe katika muktadha tofauti ambao utawaleta viongozi wa kidini na baadhi ya watu mashuhuri,” Askofu Mkuu wa Nyeri Anthony Muheria alisema.