logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kirinyaga: Mwanamke apatikana amefariki bafuni

polisi wanachunguza kifo cha mwanamke aliyefariki hamamuni

image
na

Habari25 September 2023 - 07:10

Muhtasari


• Mwili wa mwanamke huyo ulipatikana na mpangaji mwingine ambaye alikuwa ameingia bafuni.

• Mwanafamilia anayeitwa Joy Wangari alifichua kwamba mwanamke huyo alikuwa tu katika nyumba ya kukodi kwa wiki mbili.

polisi wachunguza kifo cha mwanamke Kirinyanga

Hali ya simanzi ilitanda baada ya wakaazi wa ploti moja katika mji wa Kagio, Kaunti ya Kirinyaga baada ya maiti ya mwanamke mwenye umri wa miaka 40 kugunduliwa bafuni Jumapili usiku.

Mwili wa mwanamke huyo ulipatikana na mpangaji mwingine ambaye alikuwa ameingia bafuni.

Kulingana na  walioshuhudia walisema mwanamke huyo alitumia Jumapili nzima kufagia nyumba yake.

Mwanafamilia anayeitwa Joy Wangari alifichua kwamba mwanamke huyo, mama wa watoto wawili, alikuwa tu katika nyumba ya kukodi kwa wiki mbili.

Aliongeza kuwa marehemu alikuwa amehama kutoka Nairobi na mumewe. Mimi ndiye niliyewashauri kukodi nyumba huko Kagio baada ya gharama ya juu ya maisha Nairobi.

"Yeye ni mama wa watoto wawili na amekaa hapa kwa wiki moja tu na mumewe anakuja sasa hivi kutoka Nairobi,” Wangari alisema kama ilivyoripotiwa na wanahabari Wangari alionyesha mshtuko wake mkubwa katika mabadiliko hayo ya kusikitisha.

Polisi katika kaunti ndogo ya Mwea-magharibi wanachunguza chanzo cha kifo cha mwanamke huyo.

"Tutajua sababu ya kifo chake baada ya uchunguzi wa maiti." Mwili wa marehemu ulipelekwa katika mochwari ya Kibugi ukisubiri uchunguzi wa kifo chake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved