logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gachagua hastahili kuwa naibu Rais-Raila

Raila alidai kuwa DP ameangazia eneo la kati akipuuza zingine kama vile hazipo.

image
na Radio Jambo

Makala04 October 2023 - 17:39

Muhtasari


  • Raila alisema serikali ina jukumu la kuhudumia Wakenya wote kwa usawa kwa kuwa Wakenya wote wanatozwa ushuru.

Kiongozi wa Azimio Raila Odinga amemtaka Naibu Rais Rigathi Gacgaua kuwatendea Wakenya wote kwa usawa.

Akizungumza na KTN Jumatano, Raila alisema kuwa Gachagua huwabagua Wakenya kulingana na mikoa inayodai kuwa anahudumu Mlima Kenya.

"Gachagua hastahili kuwa naibu wa rais wa Kenya kwa sababu anatoa maneno machafu ambayo inaweza kuleta kwa taifa. Yeye anasema ni naibu wa taifa la Kenya lakini yeye anajifanya naibu wa taifa la mlima Kenya," alisema.

Raila alidai kuwa DP ameangazia eneo la kati akipuuza zingine kama vile hazipo.

"Upande zile zingine za Kenya ni kigeni kwake anasema wao na sisi na anasema Kenya ni kampuni ya hisa ambapo kuna wengine wana hisa nyingi na wengine hio inaweza kugawa nchi," Raila alisema.

Aliongeza kuwa DP hafai kugawanya Wakenya kulingana na vikundi ambavyo ni vya serikali na sio.

Raila alisema serikali ina jukumu la kuhudumia Wakenya wote kwa usawa kwa kuwa Wakenya wote wanatozwa ushuru.

"Kila mtu anatozwa ushuru kwa usawa, ukitoza ushuru sukari au mafuta kila mtu analipa. Ukibagua? Hiyo ni nchi ya aina gani? Gachagua hafai kuwa DP kwa sababu ni aibu kubwa," alisema.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved