logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Esma afunguka kuhusu madai ya ugomvi na kakake Diamond

Esma alisema kuwa Diamond ni mtu mkarimu sana mara mingi hupewa zawadi naye.

image
na

Makala04 October 2023 - 13:56

Muhtasari


• "Kwa kweli kuna mengi yanasemwa kwenye mitandao, wengi wa wafuasi wetu kwenye mitandao ya kijamii wanachochea chuki kati yangu na Diamond

Baada  ya kuwa na tetesi nyingi kwenye  mitandaoni  ya kijamii  kwa muda mrefu kwake Diamond Platnumzs kutokuwa na maelewano na Dadake Esma, dadake amejitokeza kuzungumzia suala hilo.

Esma Platnumzs mfanyibiashara nchini Tanzania ambaye pia ni mtunzi wa nyimbo amefichua kuwa na uhusiano mwema na kakake mdogo ambaye ni msanii maarufu wa muziki wa Bongo Diamond Platnumz.

Kupitia kituo cha Wasafi FM kuna uvumi kinachomilikiwa Diamond walizugumza moja kwa moja na Esma Platnumz's ili kuweka wazi mambo.

"Kwa kweli kuna mengi yanasemwa kwenye mitandao, wengi wa wafuasi wetu kwenye mitandao ya kijamii wanachochea chuki kati yangu na Diamond ila yote ni uongo mimi na kakangu tuko salama na uhusiano wetu ni mema kwa hivo watu kwenye mitandao wawache kuingilia  familia ." alisema Esma.

Baada ya mwana habari kutaka kujua zaidi iwapo Diamond humtembela nyumbani kwake, Esma alisimulia kwamba wanapendana kama ndugu na dada akikiri siku ya kusherekea kuzaliwa kwa kakake Diamond walisherekea nyumbani kwake wakiwa na mama yao Mama Dangote.

"Diamond ni mtu mkarimu sana mara mingi napata zawadi kutoka kwake pia mara kwa mara tunatembeleana katika vikao vya familia ". alisema.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved