Raila amsuta Ruto baada ya kunyimwa ruhusa ya kuzuru maeneo yanayoporomoshwa Mavoko

Kinara huyo aliongeza kuwa mchakato huo ni ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu na haki za makazi ya kutosha.

Muhtasari

• Wakizungumza na vyombo vya habari alipozuru eneo hilo, viongozi wa upinzani walimkashifu Rais William Ruto kwa kuruhusu dhuluma hiyo kuendelea chini ya uangalizi wake.

• "Kinachoendelea hapa si kitendo cha kumcha Mungu. Wakati wa kampeni za Ruto mnamo Julai 2022, alikuwa ameahidi kukomesha ubomoaji haramu nchini hivi ndivyo anafanya," 

Kiongozi wa Azimio La Umoja Raila Odinga ametaja vitendo vya kufurusha watu vinavyoendelea katika Kampuni ya Saruji ya East African Portland Cement (EAPCC) kuwa vya kutomcha Mungu.

Wakizungumza na vyombo vya habari alipozuru eneo hilo, viongozi wa upinzani walimkashifu Rais William Ruto kwa kuruhusu dhuluma hiyo kuendelea chini ya uangalizi wake.

"Kinachoendelea hapa si kitendo cha kumcha Mungu. Wakati wa kampeni za Ruto mnamo Julai 2022, alikuwa ameahidi kukomesha ubomoaji haramu nchini hivi ndivyo anafanya," alisema Raila.

Kinara huyo aliongeza kuwa mchakato huo ni ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu na haki za makazi ya kutosha.

"Hii inajiri wakati serikali inasisitiza kuwa kila mtu nchini apate makazi bora. Kinachoendelea hapa kinaonyesha kutozingatiwa kwa utaratibu wa viwango vinavyotambulika vya haki za binadamu," alisema.

Aliongeza kuwa watu walioathirika zaidi ni miongoni mwa watu masikini zaidi na wanaokuja wa tabaka la kati ambao wameshuhudia akiba yao ya maisha yote ikigeuka majivu.

"Watoto wanaosoma katika baadhi ya shule hapa wameshuhudia shule zao zikipoomoshwa licha ya mitihani ya kitaifa inayokuja. Haya yanafanyika wakati tunatarajia mvua kubwa ambayo itapelekea watu kukosa makazi mbadala na mahitaji muhimu," alibainisha.

Raila aliendelea kudai kuwa kufurushwa kwa watu kutoka maeneo hayo kumeandamana na matumizi ya nguvu kupita kiasi ya polisi na mamlaka za mitaa, ambao walikuwa na nia ya kuwaumiza na kuwadhuru wanadamu.

"Kumekuwa na taarifa za majeruhi, na wizi wa mali za watu ambao wanakabiliwa na hasara."

Aliitaka serikali kuwa na mpango wa kutafuta sehemu mbadala kwa watu walioathirika.

"Kulikuwa na hamu gani ya kutumia nguvu? Kwa nini tusiwaruhusu watu watoke nje kwa amani, tuseme mwakani? Tunazungumzia watu ambao kuna uwezekano mkubwa walitumia saruji ya kampuni kujenga nyumba, baadaye kubomolewa tu na kampuni hiyo hiyo. ," alisema.

Raila alibainisha kuwa kama upinzani, hawataruhusu mchakato huo kwenda bila kupingwa.

"Unyama huu hautapita bila kupingwa, tunahitaji serikali kuchukua hatua."

Kiongozi huyo wa upinzani aliuiliwa kuingia katika majengo hayo, huku mamlaka ikitaja mchakato unaoendelea kukamilishwa kabla ya kutembelewa.

Aliandamana na Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka, Gavana wa Machakos Wavinya Ndeti, Katibu Mkuu wa ODM Edwin Sifuna, na Stewart Madzayo, miongoni mwa viongozi wengine.