Mfanyikazi wa kaunti ya Kwale, ndugu wanne wakamatwa kwa tuhuma za ufisadi wa Sh44.9m

Waliokamatwa ni pamoja na afisa mkuu wa hazina ya kaunti na kaka zake wanne.

Muhtasari

• Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma ilikubali kukamatwa na kufunguliwa mashtaka.

Mahakama
Mahakama

Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC)  siku ya Jumanne iliwakamata maafisa watano wa serikali ya kaunti ya Kwale kwa madai ya ufisadi.

Waliokamatwa ni pamoja na afisa mkuu wa hazina ya kaunti na kaka zake wanne.

Kukamatwa kwa watu hao kunahusishwa na kashfa ya ufisadi wa shilingi milioni 44.9 zinazodaiwa kuhusisha utumizi mbaya wa pesa za umma ndani ya kaunti hiyo.

Mtuhumiwa huyo anashukiwa kupanga vitendo vya rushwa, akidaiwa kuhusisha ndugu zake.

Maafisa wa EACC walidai kuwa washukiwa hao wanaaminika kutumia kampuni inayomilikiwa na familia kuwezesha ufujaji wa pesa za umma, wakihusisha sekta mbalimbali za serikali ya kaunti ya Kwale katika mchakato huo.

Washukiwa hao walisindikizwa kutoka kituo cha polisi cha Mombasa Central hadi katika Mahakama ya Kupambana na Ufisadi ili kujibu rasmi mashtaka na kukubali au kukataa mashtaka.

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma ilikubali kukamatwa na kufunguliwa mashtaka.