logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fahamu kwa nini hukumu ya Jowie Irungu imeahirishwa hadi Machi 13

Jaji Grace Nzioka alisema stakabadhi muhimu ambazo zingesaidia mahakama kufikia uamuzi wake wa mwisho ziliwasilishwa kwa kuchelewa.

image
na SAMUEL MAINA

Habari08 March 2024 - 08:19

Muhtasari


  • •Jaji Grace Nzioka alisema stakabadhi muhimu ambazo zingesaidia mahakama kufikia uamuzi wake wa mwisho ziliwasilishwa kwa kuchelewa.
, ambaye alipatikana na hatia katika mauaji ya mfanyabiashara Monica Kimani, akisubiri kuhukumiwa katika Mahakama ya Milimani mnamo Machi 8, 2024.

Mhusika mkuu wa mauaji ya mfanyibiashara Monica Irungu, Joseph Irungu almaarufu Jowie atajua hatima yake siku ya Jumatano wiki ijayo, Machi 13,  baada ya mahakama kuahirisha hukumu yake siku ya Ijumaa.

Jaji Grace Nzioka ambaye amekuwa akishughulikia kesi hiyo nzito alitoa uamuzi huo baada ya kubaini kuwa stakabadhi muhimu ambazo zingeweza kusaidia mahakama kufikia uamuzi wake wa mwisho ziliwasilishwa kwa kuchelewa.

Mahakama Kuu ilitarajiwa kutoa hukumu yake dhidi ya Jowie siku ya Ijumaa, Machi 8, baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya Monica.

Hii ni baada ya kupatikana na hatia ya mauaji katika uamuzi uliotolewa na Jaji Grace Nzioka mnamo Februari 9, na kuhitimisha kesi ya mauaji iliyoanza mwaka wa 2018.

Mahakama ya Nairobi iliamua kwamba upande wa mashtaka ulitoa ushahidi wa kutosha na kuthibitisha bila shaka kwamba Jowie alimuua Monica.

Mwanahabari Jacque Maribe, ambaye alishtakiwa pamoja na Irungu, hata hivyo aliondolewa mashtaka ya mauaji, huku hakimu akisema kuwa shtaka la mauaji sio shtaka sahihi ambalo upande wa mashtaka ungependekeza dhidi yake.

“Baada ya kuzingatia ushahidi uliotolewa upande wa mashtaka umetoa ushahidi wa kutosha na umedhihirisha kuwa mtuhumiwa alitekeleza mauaji,” Hakimu Grace Nzioka alisema katika uamuzi wake.

Katika kesi ya Maribe, hakimu aliamua kwamba ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka dhidi yake haukumweka katika nyumba ya marehemu usiku wa mauaji hatua iliyopelekea aondolewe mashtaka ya mauaji.  

Jaji huyo hata hivyo alisema kwamba Maribe alikosea kutoa taarifa za uongo kwa maafisa wa upelelezi. Kuhusiana na kosa hili, hakimu alisema kuwa ni jukumu la afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma kuamua ni hatua gani ichukuliwe dhidi yake


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved