logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Achana na siasa za Mlima Kenya! - Gachagua awazomea viongozi wa Bonde la Ufa

Gachagua amewataka viongozi wa Bonde la Ufa kuachana na siasa za Mlima Kenya akisema ni ngumu sana kwao kuzishughulikia.

image
na Radio Jambo

Habari26 May 2024 - 05:50

Muhtasari


•Gachagua amewataka viongozi wa Bonde la Ufa kuachana na siasa za Mlima Kenya akisema ni ngumu sana kwao kuzishughulikia.

akitangamana na wanawake wakati wa mpango wao wa kuwawezesha katika Kesses, kaunti ya Uasin Gishu Jumamosi, Mei 25, 2024.

Naibu Rais Rigathi Gachagua amewataka viongozi wa Bonde la Ufa kuachana na siasa za Mlima Kenya akisema ni ngumu sana kwao kuzishughulikia.

Naibu rais ambaye alikuwa akizungumza wakati wa kuchangisha fedha kwa ajili ya mpango wa kuwawezesha wanawake katika eneo la Kesses, Uasin Gishu, alishutumu baadhi ya viongozi kwa kupanga njama kubainisha ni viongozi wagani wafuatao katika Mlima Kenya.

Lakini katika onyo la wazi kwa viongozi hao, Naibu Rais alisema jitihada zao ni ubatili kwani siasa za Mlima Kenya ni ngumu zaidi kuliko wanavyofikiri.

"Mimi naomba watu wa bonde la ufa, tafadhali, sisi tuliunga Rais kwa hiari yetu na kwa kupenda na tunaendelea kumuunga mkono. Tunaomba heshima kidogo, msijaribu kutupangia siasa ya Mlima Kenya na kuptupangia uongozi," Gachagua alisema.

Gachagua alisema viongozi wa Bonde la Ufa wanapaswa kuzingatia siasa za eneo lao badala ya Mlima Kenya na kuongeza kuwa kamwe hawatafikiria kuchagua viongozi wa eneo hilo.

Naibu Rais aliwataka viongozi wa Bonde la Ufa kuangazia kumsaidia Rais William Ruto kutimiza ahadi zake za kampeni akisema kuendelea kuhusika katika siasa kutamfanya kushindwa.

Alikashifu kundi la viongozi kutoka eneo hilo na Mlima Kenya kwa kupanga njama za kumrithi Rais badala ya kulenga kumsaidia kufanikisha.

“Kumchagua kiongozi ni jambo moja na kufanikiwa ni sehemu ngumu, mimi nikiwa msaidizi mkuu wa Rais, jukumu langu ni kuhakikisha anafanikiwa, hilo ndilo lengo langu kwa sasa,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved