logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waandamanaji wapanga zaidi ya majeneza 10 CBD Nairobi

Baadhi ya maafisa walionekana wakiondoa masanduku hayo

image

Habari02 July 2024 - 12:00

Muhtasari


  • Waandamanaji walionekana wakiwa wamebeba majeneza hayowalipokuwa wakiyapanga eneo la CBD.

Waandamanaji Jumanne walijitokeza na zaidi ya majeneza 10 katika Wilaya ya Biashara ya Kati ya Nairobi.

Waandamanaji walionekana wakiwa wamebeba majeneza hayowalipokuwa wakiyapanga eneo la CBD.

Waliposogea mbali na polisi, walibeba majeneza  huku wakiwa wameyafunika kwa Bendera za Kenya.

Baadhi ya maafisa walionekana wakiondoa masanduku hayo huku waandamanaji wakiyarudisha barabarani.

Wengine walitangulia kufungua kasha huku wakipambana na polisi waliokuwa wakirusha mabomu ya machozi kuwatawanya vijana hao.

Ni maandamano ambayo yameingia wiki ya tatu huku Gen Z wakipinga mswada wa fedha.

Waandamanaji mjini Mombasa wameweza kuteketeza gari.

Mengi yafuata;

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved