logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Orodha ya hatua ambazo Rais Ruto ametoa kupunguza matumizi ya serikali

Ruto alifanya matangazo hayo wakati wa hotuba yake ya siku ya Ijumaa katika ikulu kuu ya Nairobi.

image
na SAMUEL MAINA

Habari05 July 2024 - 11:44

Muhtasari


  • •Ruto alifanya matangazo hayo wakati wa hotuba yake ya siku ya Ijumaa katika ikulu kuu ya Nairobi.

Rais William Ruto ametangaza hatua kadhaa ambazo serikali yake itachukua ili kupunguza matumizi ya fedha za serikali.

Ruto alifanya matangazo hayo wakati wa hotuba yake ya siku ya Ijumaa katika ikulu kuu ya Nairobi.

Katika hotuba yake, alisema kufuatia mashauriano mapana wameafikiana kupunguza gharama mbalimbali zikiwemo;

Kufunga angalau mashirika 47 ya serikali yenye huduma zinazoambatana.ii) Kusimamishwa kazi kwa Makatibu Tawala Wakuu (CAS).

iii) Kupunguza washauri serikalini kwa angalau asilimia 50 mara moja.

iv) Kuondoa Bajeti katika Ofisi za Mke wa Rais, Mke wa Naibu Rais na Mke wa Waziri Mkuu.

v) Bajeti za siri katika Ofisi ya Urais pia zimeondolewa.

vi) Bajeti ya ukarabati serikalini itapunguzwa kwa asilimia 50.

vii) Watumishi wa Umma watakaofikisha umri wa miaka 60 watatakiwa kustaafu mara moja na hakuna nyongeza itakayoruhusiwa.

viii) Kusimamisha ununuzi wa magari mapya serikalini kwa mwaka mmoja, isipokuwa kwa vyombo vya ulinzi na usalama.

ix) Usafiri wote usio wa lazima wa maafisa wa serikali pia umesitishwa.

x) Hakuna afisa wa serikali au mtumishi wa umma atakayeshiriki katika Harambee.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved